NEMC Kanda ya Kaskazini yafanya ukaguzi kiwanda cha kutengeneza Saruji cha Moshi Cement kinachoendeshwa na Kampuni ya JUN YU INVESTMENT INTERNATIONAL CO. LTD kilichopo katika Mkoa wa Kilimanjaro karibu na mpaka wa Horiri.
Timu ya ukaguzi ilibaini kuwa Kiwanda hicho kina cheti cha TAM, pia kina teknolojia madhubuti ya kudhibiti vumbi na kiwanda chote kimesakafiwa (paved). Hata hivyo kulikuwa na changamoto chache hasa namna ya udhibiti wa chuma chakavu na usimamizi usiofaa wa madumu yaliyomaliza kemikali.
Timu ya wataalam ilitoa maelekezo stahiki na muda wa utekelezaji ili kukabiliana na changamoto zilizoibuliwa wakati wa ukaguzi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni