Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mei 29, 2026 limeadhimisha miaka arobaini (40) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1986.
Maadhimisho hayo yamewakutanisha Viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania pamoja na wadau kutoka taasisi za umma na binafsi pamoja na mabalozi wa Mazingira ambayo yamekuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu katika suala zima la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira.
Akizungumza katika Maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi alisema miaka arobaini (40) ya NEMC ni hatua mpya ya kutekeleza majukumu kwa nguvu mpya na ufanisi, amesema katika miaka yote hiyo Baraza limejufunza, limeimarika na lipo tayari kuendelea kulitumikia Taifa kwa weledi na uzalendo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni