Timu ya watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanaofanya ukaguzi wa mazingira katika mikoa ya Kanda ya Ziwa Victoria, wakiongozwa na Meneja wa Utekelezaji wa Sheria, Mha. Luhuvilo B. Mwamila, waliadhimisha Sikukuu ya Wafanyakazi- Meimosi 2026 kwa kupanda miti katika Makumbusho ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Butiama.
Hatua hiyo ni ishara ya kuenzi dira ya Baba wa Taifa katika kuhifadhi mazingira na kusimamia utekelezaji wa sheria za utunzaji wa rasilimali za Taifa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni