Nyumbani

NEMC MBIONI KUANZISHA MASHIRIKIANO NA QATAR


Ujumbe toka Tanzania  wakiwa kwenge kikao cha pamoja na Wawakirishi wa Makampuni mbalimbali yanayojihusisha na utunzaji wa Mazingira

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar wameshiriki mikutano mbalimbali yenye lengo la kuanzisha mashirikiano katika masuala mbalimbali ya Mazingira na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kubadilishana uzoefu.

Akizungumza na ujumbe toka Tanzania, Katibu Mkuu wa Wizara ya  Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi wa nchini Qatar, Mhe. AbdulAziz Ahmad Abdullah Al-Mahmoud amesema  majukumu ya kisheria ya Wizara yake ya Mazingira yanafanana na majukumu ya NEMC hivyo, kuna kila sababu ya kushirikiana hasa katika suala zima la usimamizi wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi.

Ujumbe wa Tanzania na Qatar wakibadilishana mawazo juu ya utunzaji wa Mazingira

Wengine walioshiriki katika mikutano hiyo ni Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira toka katika Mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Mtwara kwa ajili ya kujifunza namna bora ya kusimamia mifumo ya maji taka kwa ajili ya kulinda mazingira na viumbe kwa ujumla. Vile vile ujumbe huo wa Tanzania uliweza kufanya mikutano na Taasisi nyingine ikiwemo Public Works Authority waliokuwa wanahusika na miundombinu na mifumo ya maji taka, Qatar General Electric and Water Cooperation  wanaohusika na uzalishaji na usambazaji wa  maji safi na umeme. Mikutano mingine ambayo NEMC imeshiriki ni pamoja na Qatar Foundation ambao wameonyesha utayari wa kufanya mashirikiano makubwa nchini hasa katika eneo la uhifadhi wa Ziwa Victoria hususani katika kufanya tafiti juu ya  uondoshwaji wa gugu maji vamizi lililoshamiri kwa sasa linalosababishwa na ongezeko la virutubisho majini vinavyotokana na shughuli za kibinadamu

Naye Balozi wa Tanzania nchini Qatar Mhe. Habibu Awesi Mohammed amewashukuru NEMC na Mamlaka za maji toka Dar es Salaam, Dodoma na Mtwara kuonesha utayari wa kujifunza na kushirikiana na Qatar katika suala zima la uhifadhi wa mazingira  na  usimamizi bora wa mifumo ya maji safi na taka kwa ajili ya maendeleo ya sasa na ya vizazi vijavyo

Uoto wa Asili Katika Shimo la Mungu – Hazina ya Kijani ya Newala, Mtwara

Uoto waasili katika shimo la Mungu halmashauri ya Mji Newala mkoa wa Mtwara



Katika mandhari ya kuvutia ya Kusini mwa Tanzania, ndani ya Halmashauri ya Mji Newala mkoani Mtwara, kuna eneo la kipekee linalojulikana kama Shimo la Mungu – mahali pa asili palipojaa uzuri wa kuvutia na utulivu wa asili. Eneo hili limekuwa kimbilio la uoto wa asili, likiwakilisha moja ya mifano bora ya mazingira yanayohifadhiwa na bado hayajaguswa na shughuli nyingi za kibinadamu.

Mazingira ya Shimo la Mungu

Shimo la Mungu ni bonde kubwa lenye miteremko ya kijani kibichi, milima midogo iliyozungukwa na vichaka, nyasi ndefu, na miti ya asili inayomea kwa ustawi mkubwa kutokana na hali ya hewa ya mvua na joto la wastani. Picha za mandhari ya eneo hili zinaonyesha anga lenye mawingu meupe yanayochanganyika na bluu ya anga, yakionyesha hali nzuri ya hewa na usafi wa mazingira.

Shimo la Mungu ni bonde kubwa lenye miteremko ya kijani kibichi, milima midogo iliyozungukwa na vichaka, nyasi ndefu, na miti ya asili inayomea kwa ustawi mkubwa kutokana na hali ya hewa ya mvua na joto la wastani


Uoto wa Asili na Aina za Mimea

Katika eneo hili, uoto unaojitokeza ni wa aina mbalimbali, ukiwemo:

  • Miti ya asili ya kanda ya joto inayostahimili hali ya ukame na mvua.

  • Majani marefu ya nyasi, yanayokuwa kwa wingi na kutoa makazi kwa viumbe wa aina mbalimbali.

  • Maua madogo ya njano na meupe, yanayochanua katika nyakati tofauti za mwaka na kuongeza mvuto wa kiasili wa eneo hilo.

Uoto huu wa asili ni muhimu si tu kwa uzuri wa mandhari, bali pia kwa kulinda udongo dhidi ya mmomonyoko, kuhifadhi vyanzo vya maji, na kuwa makazi ya wanyama wa porini pamoja na viumbe wadogo wa kipekee katika ukanda wa Kusini.

Umuhimu wa Kihistoria na Kiutamaduni

Shimo la Mungu pia lina umuhimu wa kiutamaduni na kihistoria miongoni mwa jamii za Newala. Wazee wa mila hulitambua kama eneo la kiroho na kimapokeo, ambapo enzi za kale lilihusishwa na imani za asili. Hii huongeza thamani ya eneo hili si tu kama kivutio cha kiasili, bali pia kama urithi wa kiutamaduni wa watu wa Mtwara.



NEMC YAENDELEA KUTOA ELIMU YA MAZINGIRA KATIKA MAONESHO YA SABASABA

Maafisa wa NEMC wakiendelea na kutoa mafunzo ya Mazigira kwenye maonesho ya SabaSaba 2025

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linaendelea kutoa elimu na huduma mbalimbali za mazingira katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Afisa wa NEMC akiendelea kutoa elimu ya mazingira kwa wageni waliotembelea banda la NEMC kwenye maonesho ya SabaSaba 2025

Ikiwa leo ni siku ya nne tangu kuanza kwa maonesho hayo, NEMC inaendelea kuwahamasisha wananchi kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira, madhara ya uchafuzi wa mazingira, pamoja na kusisitiza wananchi, wawekezaji na wafanyabiashara kutekeleza matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira.

Wageni kutoka nje ya nchi walifika kwenye banda la NEMC kupata elimu ya mazingira katika maonesho ya SabaSaba 2025

Katika banda la NEMC, wananchi wanapata fursa ya kuuliza maswali na kupata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Baraza, na namna bora ya kudhibiti taka na kelele kwenye maeneo ya makazi na biashara.

Baraza linaendelea kuwakaribisha wananchi wote kutembelea banda lake ili wapate maarifa sahihi yatakayowawezeshakuwa sehemu ya watetezi wa mazingira kwa maendeleo endelevu ya taifa letu.

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA WA USIMAMIZI WA KEMIKALI – URUGUAY 2025

Wajumbe wa NEMC wakiwakilisha Tanzania kenye mkutano wa Usimamizi wa Kemikali Uruguay 2025

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki Mkutano wa kwanza wa Kikosi Kazi kujadili Utekelezaji wa Mfumo Mpya wa Dunia wa Usimamizi wa Kemikali (Global Framework on Chemicals - GFC) uliofanyika jijini Punta del Este, nchini Uruguay kuanzia tarehe 22 hadi 27 Juni 2025.   Aidha, Mkutano huo pia ulilenga kujadili na kuandaa mikakati ya utekelezaji, upatikanaji wa fedha, ushirikishwaji wa wadau, ufuatiliaji na tathmini ya utendaji wa nchi wanachama.  Mkutano huo uliandaliwa na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), na Tanzania iliwakilishwa na taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Mamlaka ya Usalama Mahali pa Kazi (OSHA),  pamoja na asasi ya kiraia ya Agenda for Action.


 

NEMC YAPIGA KAMBI SABASABA – YAWAKARIBISHA WANANCHI KUPATA ELIMU YA MAZINGIRA

 

Mhandisi Mwandamizi wa NEMC, Bw. Haji Kiselu akizungumza katika maonyesho ya sabababa.

    Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba kwa kutoa elimu ya uhifadhi wa mazingira kwa wananchi wanaotembelea banda la lake lililopo katika Jengo la Karume.
    Akizungumza katika maonesho hayo, Mhandisi Mwandamizi wa NEMC, Bw. Haji Kiselu, amesema kuwa Baraza limejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa elimu ya mazingira inamfikia kila mwananchi, ili waweze kuelewa majukumu yao pamoja na Sheria inayolipa Baraza mamlaka ya kusimamia mazingira nchini.
    Kwa upande wake, Mhandisi wa NEMC, Bw. Peres Ntinginya, amesisitiza kuwa utunzaji wa mazingira ni jukumu la kila mmoja, na ametoa wito kwa wananchi kutumia nishati safi ya kupikia kwa kuwa matumizi yake husaidia kulinda afya ya binadamu na viumbe hai, kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa, pamoja na kuhifadhi mazingira kwa ujumla.
    Naye mmoja wa wageni waliotembelea banda la NEMC, Mkazi wa Rufiji, Bw. Ayubu Njanja, amesema elimu aliyoipata kutoka kwa Maafisa wa Baraza imempa mwongozo sahihi wa kuzingatia utunzaji wa mazingira hasa katika shughuli za kilimo.
    NEMC inaendelea kutoa wito kwa wananchi kutembelea banda lake lililopo katika Jengo la Karume, Sabasaba, Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam, ili kupata elimu ya mazingira. Maonesho haya yanafanyika kuanzia tarehe 28 Juni hadi 13 Julai 2025, yakiwa na kaulimbiu isemayo: “Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa – Fahari ya Tanzania.”
 

Mwananchi akifurahia mafunzo ya mazingira kutoka NEMC Sabasaba! Hii ni hatua kubwa kuelekea maisha bora na mazingira yenye afya. #MazingiraBora #NEMC


NEMC Sabasaba inawakaribisha wananchi kupata elimu ya mazingira kwa njia ya furaha na ushirikiano. Mazingira bora, maisha bora! #NEMC #ElimuKwaWananchi


SIMBACHAWENE AFUNGUA RASMI MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Waziri Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mh. George Simbachawene akizungumza katina maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma.

Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala bora Mhe. George Boniface Simbachawene amezindua rasmi Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma ambayo yameambatana na maonesho yatakayofanyika kuanzia leo 17-23 Juni, 2025 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
Akizungumza mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho hayo Mhe. Waziri Simbachawene amesema kwa sasa kila mmoja ni shahidi wa mageuzi katika utendaji kazi ambapo mifumo mbalimbali ya kidigitali imeanzishwa na kurahisisha utendaji kazi na upatikanaji wa taarifa. 

Washiriki katika ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma.

Watumishi wa Umma wakifuatilia kwa makini hotuba za uzinduzi, wakijizatiti kuleta mabadiliko chanya katika huduma za umma.
Picha ya pamoja ya viongozi walioshiriki uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma.

    Waziri amebainisha baadhi ya mifumo ya kidigitali iliyoleta mageuzi katika utendaji ikiwa ni pamoja na mfumo e-Watumishi ambao umeleta ufanisi katika uandaaji wa mishahara na watumishi kupata haki zao kwa wakati,  Mfumo wa Usimamizi wa Utendaji Kazi (e-Utendaji-PEPMIS) ambapo kila mtumishi wa umma anatakiwa kujaza utekelezaji wa shughuli anazofanya kila siku au kila wiki. 

    Pia mfumo wa Tathmini ya mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma (HR Assessment) unaowezesha kutambua mahitaji ya rasilimaliwatu katika utumishi wa umma na kuwafanya msawazo; na mfumo wa e-Mrejesho unaosaidia watumishi na wananchi kwa jumla kuwasilisha maoni, mapendekezo, kero na maulizo kwa Serikali haraka.

    Kwa upande wake Kaimu Meneja Kanda ya kati (NEMC) Bw. Novatus Mushi amesema katika maonesho hayo NEMC imejipanga kutoa elimu ya Mazingira na kuonesha huduma ambazo Baraza linazitoa kama ilivyo ada kuwa Siku hii hujikita kutoa elimu, kuonesha, kutoa huduma mbalimbali na kutoa fursa kwa wananchi kutoa maoni, mrejesho na changamoto mbalimbali zinazowakumba.

    Kaulimbiu iliyobeba Maadhimisho ya Wiki ya utumishi wa umma kwa mwaka 2025 ni "𝐇𝐢𝐦𝐢𝐳𝐚 𝐦𝐚𝐭𝐮𝐦𝐢𝐳𝐢 𝐲𝐚 𝐦𝐢𝐟𝐮𝐦𝐨 𝐲𝐚 𝐤𝐢𝐝𝐢𝐠𝐢𝐭𝐚𝐥𝐢 𝐢𝐥𝐢 𝐤𝐮𝐨𝐧𝐠𝐞𝐳𝐚 𝐮𝐩𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚𝐧𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚 𝐭𝐚𝐚𝐫𝐢𝐟𝐚 𝐧𝐚 𝐤𝐮𝐜𝐡𝐚𝐠𝐢𝐳𝐚 𝐮𝐰𝐚𝐣𝐢𝐛𝐢𝐤𝐚𝐣𝐢"

    Aidha, chimbuko la Sherehe hizi ni uamuzi wa Mkutano wa Mawaziri wenye dhamana ya Utumishi wa Umma uliofanyika mjini Tangiers Nchini Morocco mwaka 1994. Uamuzi huo ulizitaka Nchi za Afrika kusherehekea siku hii kwa kaulimbiu moja katika Bara zima la Afrika




 

"MAZINGIRA CHALLENGE: UKO WAPI TANZANIA?" HIZI HAPA PICHA ZA WADAU

 

Msitu wa Kagunga  uliopo kijiji cha Kagunga  kata ya Kasekese wilaya ya Tanganyika mkoa wa Tatavi zimepigwa na Mawiti

Ufukwe wa bahari ya jange kata ya Kitumbikwela Halmashauri ya Manispaa ya LINDI, ni maarufu kwa kiliomo cha zao la mwani zimepigwa na Wawawa

Bonde la mpunga  katika kijiji cha Ifinsi Halmashauri ya wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi,maji hutiririka  msimu wote wa mwaka imepigwa na Paulogchomba

Hapa ni Tarime vijijini-Mkoa wa Mara picha na aboy

Ufukwe wa bahari ya Lindi mjini Picha na Wawawa

Bonde Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya na Mbarali picha na Ndemba - MOI




Mazingira kutoka Hifadhi ya mto Ugalla unapotikana wilayani Kaliua Mkoa wa Tabora




Sethi Ura Company Limited Yasimamia Mapinduzi ya Usafi: Ushirikiano wa Jamii Katika Kuweka Mazingira Safi Hospitali ya Wilaya ya Hai

Vijana wa kujitolea wakipanga majukumu kabla ya kuanza kazi ya usafi katika eneo la hospitali. Katika kuendeleza dhana ya afya bora inayoteg...