Nyumbani

NEMC YAJA NA USAFI KAMPENI 2025

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limezindua kampeni mpya ya usafi iitwayo "NEMC Usafi Kampeni' 2025" yenye lengo la kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika usafi wa mazingira na kuhakikisha nchi inakuwa safi, salama na yenye afya kwa wote.

Kampeni hiyo ambayo itatekelezwa kwa ushirikiano na Ofisi ya Rais - TAMISEMI, mamlaka za mikoa na Halmashauri, Taasisi binafsi, Asasi zisizo za kiserikali na wananchi, inalenga kuibua mabadiliko ya tabia na kukuza uwajibikaji wa pamoja katika kudhibiti ongezeko la uchafuzi wa mazingira, hasa taka ngumu na plastiki.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na utekelezajinwa Sheria NEMC Bw. Jamal Baruti, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu alisema kwa sasa Tanzania inazalisha takriban tani milioni 14.4 hadi 20.7 za taka kwa mwaka, huku wastani wa uzalishaji taka kwa mtu mmoja ukiwa kati ya kilo 0.66 hadi 0.95 kwa siku. Hali hii inahitaji jitihada za dhati kutoka kwa kila mtanzania.

"Kampeni hii inalenga kuondoa dhana kuwa usafi ni jukumu la serikali pekee. Kila mtu anapaswa kushiriki, kwa kuwa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 inamtaka kila mtu kuwa mdau na mlinzi wa mazingira," alisema Baruti.

Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti akizungumza na Vyombo vya habari katika Uzinduzi wa Kampeni hiyo

Aliongeza kuwa kampeni hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050, ambayo imeweka hifadhi ya mazingira kuwa moja ya mihimili ya maendeleo endelevu. Kupitia kampeni hii, taka zitatazamwa kama fursa ya ajira kupitia miradi ya kijani, vijana na wanawake watawezeshwa kupitia mafunzo ya ujasiriamali wa mazingira, huku upandaji miti ukihamasishwa kwa nguvu zote.

Miongoni mwa shughuli zitakazofanyika chini ya kampeni hiyo ni pamoja na operesheni za usafi, mafunzo ya elimu ya mazingira, mashindano ya usafi kwa shule na kata, uanzishaji wa bustani za kijani, maonesho ya bidhaa rafiki kwa mazingira, pamoja na uanzishwaji wa klabu za mazingira katika shule zote za msingi na sekondari ifikapo Juni 2026.

Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na utekelezajinwa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti akizungumza na Vyombo vya habari katika Uzinduzi wa Kampeni hiyo

Meneja wa Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bw. Hamad Taimuru (kushoto) akielezea jambo wakati  wa uzinduzi wa "NEMC Usafi Kampeni"..

NEMC YAWANOA MAWAKILI WA SERIKALI SHERIA YA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa mafunzo ya uelewa wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira na utekelezaji wa majukumu yake kwa mawakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.

Akizungumza katika Mafunzo hayo tarehe 3 Septemba, 2025 Mkurungenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Semesi amesema kuwa wameandaa mafunzo hayo kwa lengo la kujengeana uelewa wa kisheria katika usimamizi wa mazingira nchini pamoja na kuboresha mahusiano mazuri katika Usimamizi na Utekelezaji wa Sheria za Mazingira nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akizungumza katika Mafunzo hayo 

Akifungua Mafunzo hayo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amesema wanasheria hao wanatakiwa kuwa walinzi na kuongeza umakini katika kutoa ushauri wa sheria za mazingira kwa maslahi ya nchi.

"Natambua zipo changamoto wakati wa utekelezaji, mfano uelewa mdogo wa masuala ya mazingira hivyo tunawajibu wa kuzibadili changamoto hizi na kuzifanya fursa kwa kuimarisha nafasi ya NEMC katika kusimamia sheria katika sekta ya mazingira."Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali amelishukuru Baraza na kueleza kuwa mafunzo hayo yataongeza uelewa kwa Mawakili wa Serikali hivyo kuwasaidia wakati watakapokuwa wanatoa Ushauri wa Kisheria na Upekuzi wa Mikataba inayohusu hifadhi na usimamizi wa mazingira nchini.

Baadhi ya Mawakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria wakifuatilia mafunzo hayo

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari akieleza jambo wakati wa Mafunzo hayo
Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akimweleza jambo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari mara baada ya Mafunzo hayo, Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Utawala na Fedha (NEMC) Bw. Dickson Mjinja na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Sheria NEMC, Bw. Joannes Karungura 

Picha ya pamoja mara baada ya mafunzo hayo

NEMC YAJENGEWA UWEZO KUPITIA MAFUNZO YA KIMATAIFA KUHUSU UFADHILI WA MIRADI YA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na African Adaptation Initiative (AAI), limeandaa warsha ya siku tatu kwa ajili ya kuwajengea uwezo wataalamu wake kuhusu mbinu bora za kupata na kusimamia fedha za miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambayo inafanyika kuanzia 26-28 Agosti, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa NEMC.

AAl, ambayo ilianzishwa na Wakuu wa Nchi za Afrika, inalenga kusaidia mataifa ya Bara la Afrika katika kuongeza uwezo wao wa kupata rasilimali za kifedha za kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.


Baadhi ya wajumbe kutoka  African Adaptation Initiative (AAI) wakiwasilisha mada katika Warsha hiyo

Kupitia mpango wake mahsusi uitwao Adaptation Project Incubator for Africa (APIA), AAl inasaidia taasisi na nchi wanachama kuboresha uandishi, uandaaji na utekelezaji wa miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Aidha, NEMC iliingia makubaliano ya ushirikiano (MoU) na AAl ili kuwezesha Tanzania kunufaika na fursa hii ya mafunzo. Warsha hii ni matokeo ya makubaliano hayo na inalenga kuimarisha uelewa wa wataalamu wa NEMC katika maeneo mbalimbali ikiwemo: Mifumo ya kitaasisi na kifedha kuhusu mabadiliko ya tabianchi, Uandishi na uwasilishaji wa Miradi ya kimataifa, Usimamizi wa utekelezaji wa miradi, na mbinu za kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya kimataifa kuhusu fedha za miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.


Watumishi wa Baraza wakichangia mada katika Warsha hiyo

Baadhi ya Watumishi wa Baraza wakifuatilia mafunzo ya Warsha hiyo





Picha ya pamoja mara baada ya kuhitimishwa kwa Warsha ya siku tatu yakuwajengea uwezo wataalamu wa NEMC kuhusu mbinu bora za kupata na kusimamia fedha za miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi iliyofanyika kuanzia 26-28 Agosti, 2025 

Kupitia mpango wake mahsusi uitwao Adaptation Project Incubator for Africa (APIA), AAl inasaidia taasisi na nchi wanachama kuboresha uandishi, uandaaji na utekelezaji wa miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Aidha, NEMC iliingia makubaliano ya ushirikiano (MoU) na AAl ili kuwezesha Tanzania kunufaika na fursa hii ya mafunzo. Warsha hii ni matokeo ya makubaliano hayo na inalenga kuimarisha uelewa wa wataalamu wa NEMC katika maeneo mbalimbali ikiwemo: Mifumo ya kitaasisi na kifedha kuhusu mabadiliko ya tabianchi, Uandishi na uwasilishaji wa Miradi ya kimataifa, Usimamizi wa utekelezaji wa miradi, na mbinu za kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya kimataifa kuhusu fedha za miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Kupitia mafunzo haya, NEMC inatarajiwa kuongeza uwezo wake wa kuandaa na kusimamia miradi mikubwa ya kimkakati, hivyo kuisaidia Tanzania kuongeza fursa za kupata fedha za kimataifa kwa ajili ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

NEMC YASHIRIKI KONGAMANO LA PIKA KIJANJA 2025 – UBUNGO PLAZA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) leo 22 Agosti, 2025 limeshiriki  Kongamano la Pika Kijanja lililoandaliwa na TBC pamoja na Bongo FM ambalo ni sehemu ya Kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati safi ya kupikia.

Kongamano hilo limefanyika katika Ukumbi wa Ubungo plaza ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila akizungumza katika Kongamano hilo

Akizungumza, mgeni katika Kongamano hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  mhe. Albert Chalamila, amesema jamii ikiendelea kutumia nishati chafu ya kupikia itahatarisha usalama wa vizazi vijavyo kutokana na uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya nishati hiyo, jambo ambalo ameliita ni usaliti wa dunia ijayo. 

Katika Kongamano hilo NEMC pia imeshiriki majadiliano yaliyolenga kuelimisha na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa matumizi ya Nishati safi ya kupitia ikiwemo gesi na pia kuelimisha kuhusu madhara ya Nishati chafuzi kwa Afya na Mazingira.

Baadhi ya Maafisa wa NEMC katika Kongamano hilo

Kongamano hili lililowakutanisha wadau mbalimbali wa Nishati na Mazingira wakiwemo wanawake linafanyika kwa mara ya tano tangu kampeni ya Pika Kijanja ilipoanzishwa mwaka 2022


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila (wa pili kulia) na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo

𝐁𝐎𝐃𝐈 𝐘𝐀 𝐍𝐄𝐌𝐂 𝐘𝐀𝐍𝐎𝐋𝐄𝐖𝐀 𝐌𝐅𝐔𝐌𝐎 𝐖𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐀𝐓𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐀𝐙𝐈𝐍𝐆𝐈𝐑𝐀 𝐊𝐈𝐃𝐈𝐉𝐈𝐓𝐀𝐋𝐈


Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) imepitishwa kwenye wasilisho maalum kuhusu Mfumo wa Kidijitali wa Kufuatilia Uchafuzi wa Mazingira ujulikanao kama Online Continuous Emissions Monitoring System (OCEMS).

Mfumo huu wa kisasa umeundwa kwa lengo la kufanikisha ufuatiliaji wa wakati halisi wa viwango vya uchafuzi vinavyotolewa na viwanda na sekta mbalimbali, hatua inayolenga kuongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika kusimamia mazingira nchini.

Kupitia mfumo huu, taarifa za uchafuzi wa hewa zitapatikana moja kwa moja na kwa wakati  jambo ambalo litasaidia katika kufanya uamuzi sahihi kuhusu hatua za kudhibiti uchafuzi. Aidha, mfumo huu utawezesha kuimarika kwa ushirikiano kati ya wadau wa mazingira kwa kuwa taarifa zitakuwa wazi na zinazopatikana kwa urahisi, hivyo kuchochea jitihada za pamoja katika kulinda mazingira na afya ya jamii.


Bodi ya NEMC ikipatiwa Mafunzo ya mfumo wa ufuatiliaji wa Mazingira Kidigitali

NEMC YAFANIKISHA MAFUNZO YA KUJENGEA UWEZO KITAIFA WIZARA, TAASISI NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA JUU YA NYENZO ZA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza za la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC limefanikisha mafunzo ya kujenga uwezo wa kitaifa juu ya nyenzo za Usimamizi wa Mazingira nchini kwa Wizara, Taasisi na Mamlaka za Serikali za mitaa.

Mafunzo hayo ya siku mbili   yalianza jana 20 Agosti, hadi leo 21, 2025 katika Hoteli ya Midland Jijini Dodoma huku yakihusisha uwasilishaji wa mada na majadiliano, pamoja na maswali na majibu ya papo kwa papo.

Aidha mafunzo hayo yalilenga kuhakikisha Taasisi zote za umma na Mamlaka za Serikali za mitaa zinahakikisha matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake yanatekelezwa ipasavyo


Afisa Mazingira Mkuu wa NEMC na Mratibu Mkuu wa Mradi wa EMA upande wa NEMC, Bw. Paul Mashaija Kalokola akizungumza katika Mafunzo hiyo

Baadhi ya mada zilizowasilishwa ni pamoja na hali ya udhibiti wa taka za kielekroniki katika miji na manispaa, changamoto na fursa zilizopo katika taka za kielektroniki,  Udhibiti wa madampo haramu, Mpango mkakati wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira, Mchakato wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii pamoja na Kaguzi za Mazingira pamoja na mchakato wa kupata vibali vya taka hatarishi pamoja na changamoto zilizopo katika udhibiti wake. 


Baadhi ya maafisa wa NEMC wakiwasilisha mada katika Mafunzo hiyo

Katika kuhitimisha mafunzo hayo baadhi ya washiriki wamelishukuru Baraza kwa mafunzo hayo huku wakieleza kuwa wamepata mbinu mpya ambazo awali hawakuwa nazo katika swala zima la Usimamizi wa Mazingira nchini.



Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo

NEMC YAZITAKA TAASISI ZA UMMA KUTEKELEZA KWA UFANISI SHERIA YA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limezitaka taasisi za umma zikiwemo Wizara, Idara, Wakala wa Serikali na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake yanatekelezwa ipasavyo katika maeneo yao ya kazi.

Wito huo umetolewa leo, tarehe 20 Agosti 2025, katika semina ya mafunzo ya nyenzo za usimamizi wa mazingira chini ya Mradi wa EMA kwa Taasisi za Umma inayoendelea katika Hoteli ya Midland, Jijini Dodoma kuanzia tarehe 20 hadi 21 Agosti 2025.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, mgeni rasmi ambaye ni Meneja wa Maeneo Maalumu na Mabadiliko ya Tabianchi, Dkt. Careen Anatory Kahangwa, amesema lengo la semina hiyo ni kuimarisha mbinu za kazi na uwezo wa utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, sambamba na kuimarisha mifumo ya kisheria na kitaasisi kwa ajili ya usimamizi bora wa mazingira nchini.

Meneja wa Maeneo Maalumu na Mabadiliko ya Tabianchi (NEMC), Dkt. Careen Anatory Kahangwa akizungumza wakati wa Semina ya kujenga uwezo wa kitaifa juu ya nyenzo za Usimamizi wa Mazingira nchini kwa Wizara, Taasisi na Mamlaka za Serikali za Mitaa chini ya Mradi wa EMA.

"Ushiriki wenu katika kikao hiki ni wa muhimu kwa kuwa unalenga kuhakikisha utekelezaji wa sheria za kitaifa na mikataba ya kimataifa ya mazingira. Hii itawezekana tu iwapo mtayapokea mafunzo haya kwa umakini na kuyazingatia ili kujengewa uwezo wa kutosha katika kusimamia vyema mazingira," alisema Dkt. Kahangwa.

Kwa upande wake, Afisa Mazingira Mkuu wa NEMC na Mratibu Mkuu wa Mradi wa EMA, Bw. Paul Mashaija Kalokola ameeleza kuwa kumekuwa na uhitaji mkubwa wa kujengea uwezo taasisi mbalimbali ili wadau waweze kufahamu na kutumia nyenzo muhimu za usimamizi wa mazingira nchini.

Afisa Mazingira Mkuu wa NEMC na Mratibu Mkuu wa Mradi wa EMA upande wa NEMC, Bw. Paul Mashaija Kalokola akizungumza katika Semina hiyo

Ameongeza kuwa changamoto kubwa kwa sasa ni udhaifu wa baadhi ya taasisi katika kutekeleza ipasavyo Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, hali iliyosababisha kuanzishwa kwa mradi huo wa miaka mitatu unaosimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais, wenye lengo la kuimarisha uwezo wa wadau wote nchini katika kusimamia mazingira kwa ufanisi.

Baadhi ya washiriki wa semina ya mafunzo ya nyenzo za usimamizi wa mazingira chini ya Mradi wa EMA   





Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo wakichangia mada 


Washiriki wa Semina  ya kujenga uwezo kitaifa juu ya nyenzo za usimamizi wa Mazingira chini ya Mradi wa EMA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya awamu ya kwanza ya mafunzo hayo


NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...