Naibu Waziri wa Maji Mhe. Mhandisi Kundo Andrew Mathew amesisitiza umuhimu wa NEMC kuharakisha mifumo ya mawasiliano na tehama katika kuratibu shughuli za Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) na TISEZA kwenye upangaji wa maeneo ya uwekezaji na kuwataka kuwa na mpango kazi ulio wazi (clear roadmap) utakaoruhusu Tathmini za Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) kufanyika kwa haraka na ufanisi mkubwa, hatua itakayosaidia kuondoa urasimu na kuchochea kasi ya wawekezaji kuleta mitaji yao nchini.
Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, ameipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa ubunifu na mikakati thabiti wakati alipotembelea banda lao katika Maonesho ya Kuelekea Siku ya Mazingira Duniani.