Nyumbani

𝗨𝗦𝗜𝗠𝗔𝗠𝗜𝗭𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗭𝗜𝗡𝗚𝗜𝗥𝗔 𝗨𝗘𝗡𝗗𝗘 𝗦𝗔𝗠𝗕𝗔𝗠𝗕𝗔 𝗡𝗔 𝗨𝗞𝗨𝗔𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗨𝗪𝗘𝗞𝗘𝗭𝗔𝗝𝗜 𝗡𝗪-𝗠𝗔𝗝𝗜, 𝗠𝗛𝗔𝗡𝗗𝗜𝗦𝗜 𝗞𝗨𝗡𝗗𝗢 𝗠𝗔𝗧𝗛𝗘𝗪

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Mhandisi Kundo Andrew Mathew amesisitiza umuhimu wa NEMC kuharakisha mifumo ya mawasiliano na tehama katika kuratibu shughuli za Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) na TISEZA kwenye upangaji wa maeneo ya uwekezaji na kuwataka kuwa na mpango kazi ulio wazi (clear roadmap) utakaoruhusu Tathmini za Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) kufanyika kwa haraka na ufanisi mkubwa, hatua itakayosaidia kuondoa urasimu na kuchochea kasi ya wawekezaji kuleta mitaji yao nchini.

Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, ameipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa ubunifu na mikakati thabiti wakati alipotembelea banda lao katika Maonesho ya Kuelekea Siku ya Mazingira Duniani.



PLASTIKI HAI ILIYOTENGENEZWA KWA MABAKI YA CHAKULA YAWA KIVUTIO MAONESHO KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Mfumo wa Plastiki hai ambao ni rafiki kwa Mazingira kutoka chuo kikuu Ardhi wawa kivutio Banda la NEMC Maonesho ya Mazingira kuelekea Siku ya Mazingira Duniani.

Mfumo huu unahusisha magamba ya samaki, mabaki ya vyakula kama magamba ya mihogo, magamba ya ndizi na pumba za mpunga zinachakatwa na kutengeneza Plastiki hai ambazo ni rafiki kwa Mazingira zinazoweza kutumika kama vifungashio







NEMC YATAMBUA MCHANGO WA TFS KAMPENI YA UPANDAJI MITI NCHI NZIMA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetambua mchango wa TFS katika zoezi Zima la kampeni ya upandaji miti 40,000 nchi nzima kwa kumpatia zawadi Naibu Kamishna wa Uhifadhi (TFS) Salehe S. Beleko alipozuru Banda la NEMC viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Center ikiwa ni wiki ya Maonesho kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani yenye kaulimbiu isemayo Dira 2050- Tuwajibike kukijanisha Tanzania.






"𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗠𝗡𝗔𝗙𝗔𝗡𝗬𝗔 𝗞𝗔𝗭𝗜 𝗡𝗭𝗨𝗥𝗜" -𝗡𝗪-𝗧𝗔𝗠𝗜𝗦𝗘𝗠𝗜, 𝗗𝗞𝗧. 𝗦𝗘𝗜𝗙

Ni kauli yake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), anayeshugulikia Afya, Dkt. Rajabu Seif, alipotembelea banda la NEMC  viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre, Jijini Dodoma kwenye maonesho ya kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika 05/06 Kila Mwaka ambayo kwa mwaka huu yanakaulimbiu isemayo Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania.


Akiwa katika banda hilo, Dkt. Seif alipongeza juhudi za NEMC katika kuelimisha wananchi kuhusu masuala ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini.

Alisema kazi inayofanywa na NEMC ina mchango mkubwa katika kuongeza uelewa wa jamii kuhusu wajibu wao wa kulinda mazingira na kuhakikisha rasilimali za asili zinatunzwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.


Katika banda hilo, wananchi wanapata elimu kuhusu umuhimu wa kufanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii, umuhimu wa upandaji miti, utenganishaji wa taka kuanzia kwenye chanzo, pamoja na dhana ya taka sifuri inayolenga kupunguza uzalishaji wa taka na kuongeza matumizi ya mbinu za urejelezaji. 

Dkt. Seif alisisitiza kuwa ushirikiano kati ya NEMC, taasisi mbalimbali na wananchi ni muhimu katika kufanikisha agenda ya uhifadhi na usimamizi endelevu wa mazingira nchini inafanikiwa kwa maendeleo endelevu.

ELIMU YA MAZINGIRA IKITOLEWA KATIKA MAONESHO YA KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI JUNI 5 2026

 Elimu ya Mazingira ikiendelea kutolewa katika Banda la NEMC katika maonesho kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete (JKCC) jijini Dodoma 

Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi tarehe 1 Juni 2026 na Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa.




NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU-TAMISEMI (AFYA) MHE. DKT. RAJAB SEIF AZURU BANDA LA NEMC KATIKA MAONESHO YA KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI anayeshughulikia Afya Mhe. Dkt. Rajab Seif azuru Banda la NEMC katika maonesho ya kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo leo ni siku ya tatu tangu kufunguliwa kwake tarehe 1Juni, 2026.






WATUMISHI WA NEMC WAKITOA ELIMU YA MAZINGIRA KATIKA WIKI YA MAONESHO KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI, JUNI 2026


Elimu ya Mazingira ikitolewa katika maonesho kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete (JKCC) jijini Dodoma ambapo Maadhimisho hayo yatafanyika Juni 5.