Nyumbani

PROFESA MSOFE ARIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA NEMC

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira)  Profesa Peter  Msofe  ameonekana kuridhishwa na utendaji kazi na uwajibikaji wa watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika utekelezaji wa majukumu ya Mazingira hasa usimamizi wa utekelezaji wa Sheria ya Mazingira Nchini.

Hayo yamedhihirika wakati alipotembelea Ofisi za Baraza jijini Dar es Salaam kwa mara ya kwanza toka kuteuliwa kwake katika nafasi hiyo ya Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Mazingira.

Amesema "NEMC pamoja na changomoto zote, bado mmepiga hatua katika suala Zima la usimamizi wa utekelezaji wa Sheria ya Mazingira nchini.

Mapokezi ya Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msofe alipotembelea Ofisi za NEMC tarehe 31 Julai, 2025 Jijini Dar es Salaam

Amesema "NEMC  mnafanya kazi, watu wanaona na mnaonekana, licha ya changamoto mnazokumbana nazo, lakini endeleeni kufanya  kazi kwa ajili ya manufaa ya Taifa la Tanzania,  huku mkilinda Afya zenu dhidi ya  Mazingira hatarishi katika Utekelezaji wa majukumu yenu" amesema Prof.Msofe.

Aidha ameainisha mambo matano ambayo watumishi wa NEMC wanatakiwa  kuyazingatia katika utekelezaji wa majukumu ambayo ni kuweka uwiano kati ya vihatarishi binafsi na vihatarishi vya Mazingira ya kazi ili kuepuka madhara ya kiafya katika Utekelezaji wa majukumu, kujifunza na kushirikishana ujuzi wa utendaji kazi, ushirikiano mkubwa katika kazi na uvumbuzi katika maswala ya Mazingira ili kuweza kufanya kazi kwa kuendana na ulimwengu wa sasa

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msofe akizungumza katika kikao na watumishi alipotembelea Ofisi za NEMC tarehe 31 Julai, 2025. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Msofe akizungumza wakati wa Kikao na watumishi wa NEMC

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi alipozungumza ameesema bado NEMC inakabiliana na changamoto katika kutekeleza majukumu yake kutokana na kukosekana kwa Sheria inayotoa Mamlaka kamili ya Utekelezaji ambapo bado mchakato wa kuifanya NEMC kuwa Mamlaka unaendelea.

Amesema Baraza linatumia Vyombo vya ulinzi na usalama katika Utekelezaji wa baadhi ya majukumu kutokana na kukosekana kwa Mamlaka kamili.

Baadhi ya watumishi wa NEMC wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msofe wakati wa Kikao hicho

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msofe na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi wakifuatilia wasilisho kuhusu kazi na majukumu mbalimbali ya NEMC lililowasilishwa na mmoja wapo wa watumishi 

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akimkabidhi zawadi Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msofe mara baada ya Kikao na watumishi wa Baraza
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msofe (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa NEMC mara baada ya Kikao na watumishi. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi na kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Utawala na Fedha (NEMC) Bw. Dickson Mjinja

PROFESA MSOFE ARIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA NEMC

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira)  Profesa Peter  Msofe  ameonekana kuridhishwa na utendaji kazi na uwajibikaji wa watum...