Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Kusini limeshiriki katika Warsha ya kuelimisha umma kuhusu uwazi na uwajibikaji katika Sekta ya Uziduaji, iliyofanyika Februari 2, 2026 katika Ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, Manispaa ya Mtwara Mikindani, mkoani Mtwara.
Katika warsha hiyo, Bw. Obasanjo Nniwako (SEO) aliwasilisha mada kuhusu utunzaji wa mazingira na Uzingatiaji wa Sheria na kanuni za mazingira katika shughuli za utafiti na uchimbaji wa madini, mafuta na gesi asilia. Huku mgeni rasmi akikuwa ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Ndugu Terence Ngole, aliyemwakilisha Waziri wa Madini, Mheshimiwa Antony Mavunde.
NEMC iliwahimiza wachimbaji wa kati na wadogo, hususan kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara, kuzingatia matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake ili kuepusha athari za mazingira, huku ikisisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa kwa watakaokiuka taratibu hizo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni