𝗟𝗲𝗻𝗴𝗼 𝗻𝗶 𝗸𝘂𝗷𝗮𝗱𝗶𝗹𝗶 𝗨𝘁𝗲𝗸𝗲𝗹𝗲𝘇𝗮𝗷𝗶 𝘄𝗮 𝗧𝗮𝘁𝗵𝗺𝗶𝗻𝗶 𝘆𝗮 𝗦𝗲𝗸𝘁𝗮 𝘆𝗮 𝗠𝗮𝗱𝗶𝗻𝗶 𝗻𝗰𝗵𝗶𝗻𝗶
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikao kilichoandaliwa na Benki ya Dunia kwa kushirikiana na Wizara ya Madini kilicholenga kujadili na kupata uelewa wa pamoja kuhusu utekelezaji wa Tathmini ya Sekta ya Madini nchini inayojulikana kama Mining Sector Diagnostic (MSD)
Kikao hicho kilichofanyika tarehe 10 Machi 2026 katika ukumbi wa Hoteli ya Best Western jijini Dodoma kiliwakutanisha wadau kutoka Wizara, Taasisi na Wakala za Serikali.
Tathmini ya MSD inalenga kuchambua namna shughuli za Sekta ya madini zinavyotekelezwa na kusimamiwa, hususan kwa kuzingatia masuala ya Sheria, Kanuni, mifumo ya kikodi pamoja na uwezo wa Taasisi mbalimbali za Serikali katika kusimamia Sekta hiyo.
Matokeo ya tathmini ya MSD yataisaidia Benki ya Dunia kutambua kwa kina mchango wa Sekta ya madini katika maendeleo ya Taifa, pamoja na kubaini maeneo yanayohitaji kuboreshwa.
Kupitia matokeo hayo, mapendekezo yatatolewa kuhusu namna bora ya kuimarisha ufanisi wa Sekta hiyo kwa kufanya maboresho ya sera, mifumo ya usimamizi na kuboresha mazingira ya uwekezaji.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni