Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika tarehe 5 Juni 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma.
Maadhimisho hayo, yanayofanyika kila mwaka tarehe 5 Juni, kwa mwaka huu yaliadhimishwa kitaifa kwa kauli mbiu isemayo “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania”.
Mgeni rasmi wa hafla hiyo alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi ambapo kabla ya kilele cha Maadhimisho hayo kikitanguliwa na maonesho ya wiki nzima yaliyolenga kutoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu uhifadhi na usimamizi wa mazingira kupitia banda lake maalum.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni