Nyumbani

NEMC YAONGEZA VYOMBO VYA USAFIRI KUIMARISHA MIUNDOMBINU WEZESHI YA UTEKELEZAJI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeongeza vyombo vya usafiri kwa kutumia mapato yake ya ndani, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha miundombinu wezeshi ya utekelezaji wa majukumu ya kimazingira, ikiwemo ufuatiliaji, ukaguzi na uzingatiaji wa Sheria ya mazingira nchini.

Akizungumza leo Agosti 11, 2026 wakati wa makabidhiano ya magari mawili kwa baadhi ya viongozi wa Baraza, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, amesema Baraza limeanza na magari mawili kati ya matano kwa ajili ya viongozi na linatarajia kununua magari mengine 20 ndani ya mwaka huu kwa ajili ya kuimarisha utendaji kazi katika Kanda zote 13 nchini.


 
“Magari haya tumeyanunua sisi wenyewe kwa kutumia mapato yetu ya ndani na tunaanza na magari 5 kwa ajili ya viongozi, lakini kwa malengo tuliyojiwekea kwa mwaka huu tutanunua magari mengine 20 " amesema Dkt. Semesi.

Ameongeza “Hii ni katika kuhakikisha tunaboresha utendaji kazi katika jukumu tulilokasimiwa la usimamizi wa mazingira nchini, sawa na malengo na matakwa ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 pamoja na malengo ya Rais wetu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan,”

Naye Mkurugenzi wa Utawala na Fedha Bw. Dickson Mjinja alipozungumza aliahidi utunzwaji wa magari hayo na kutumika kwa malengo kusidiwa huku akisistiza uwajibikaji kufikia





NEMC YAWEKA MSINGI WA UTEKELEZAJI WA ESG NA URIPOTI WA UENDELEVU


Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeendelea kuimarisha uwezo wake katika masuala ya Mazingira, Jamii na Utawala Bora (Environmental, Social and Governance – ESG) pamoja na uripoti wa uendelevu, kupitia mafunzo ya siku tano yaliyotolewa na KPMG kuanzia tarehe 3 hadi 7 Agosti 2026 katika Ofisi ya Kanda ya Temeke ya NEMC, Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango endelevu wa Baraza wa kuimarisha mifumo na kanuni za ESG na kuweka uripoti wa uendelevu kuwa sehemu ya utendaji wa kitaasisi. Mpango huo unahusisha maandalizi ya Sera ya ESG, Mfumo wa ESG, pamoja na Ripoti ya Uendelevu ya Baraza kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kwa kuzingatia vipaumbele vya kitaifa na mifumo ya kimataifa inayotambulika katika uripoti wa uendelevu.


Katika mafunzo hayo, maafisa walioteuliwa kuwa Mabingwa wa ESG na Uripoti wa Uendelevu (ESG & Sustainability Reporting Champions) walipata uelewa na ujuzi wa vitendo kuhusu misingi ya ESG, mifumo ya uripoti wa uendelevu, tathmini ya masuala muhimu ya kimazingira, kijamii na kiutawala, ushirikishwaji wa wadau, usimamizi wa takwimu za ESG, pamoja na namna ya kuandaa na kuratibu uripoti wa uendelevu ndani ya taasisi.


Aidha, mafunzo hayo yameweka msingi wa kuanza kwa vikao na shughuli za vitendo vitakavyowezesha maandalizi ya Sera ya ESG, Mfumo wa ESG na Ripoti ya kwanza ya Uendelevu ya NEMC. Hatua hii inalenga kuhakikisha kuwa masuala ya ESG yanaendelea kujumuishwa katika mipango, shughuli na mifumo ya utendaji wa Baraza.


Kupitia hatua hiyo, NEMC inaendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuimarisha uhifadhi na usimamizi endelevu wa mazingira, ufanisi wa kitaasisi, uwajibikaji na uwazi, sambamba na kuchangia katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu na vipaumbele vya taifa.




NEMC YAONGEZA VYOMBO VYA USAFIRI KUIMARISHA MIUNDOMBINU WEZESHI YA UTEKELEZAJI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeongeza vyombo vya usafiri kwa kutumia mapato yake ya ndani, ikiwa ni sehemu ...