Nyumbani

NEMC YAFANIKISHA MAFUNZO YA KUJENGEA UWEZO KITAIFA WIZARA, TAASISI NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA JUU YA NYENZO ZA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza za la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC limefanikisha mafunzo ya kujenga uwezo wa kitaifa juu ya nyenzo za Usimamizi wa Mazingira nchini kwa Wizara, Taasisi na Mamlaka za Serikali za mitaa.

Mafunzo hayo ya siku mbili   yalianza jana 20 Agosti, hadi leo 21, 2025 katika Hoteli ya Midland Jijini Dodoma huku yakihusisha uwasilishaji wa mada na majadiliano, pamoja na maswali na majibu ya papo kwa papo.

Aidha mafunzo hayo yalilenga kuhakikisha Taasisi zote za umma na Mamlaka za Serikali za mitaa zinahakikisha matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake yanatekelezwa ipasavyo


Afisa Mazingira Mkuu wa NEMC na Mratibu Mkuu wa Mradi wa EMA upande wa NEMC, Bw. Paul Mashaija Kalokola akizungumza katika Mafunzo hiyo

Baadhi ya mada zilizowasilishwa ni pamoja na hali ya udhibiti wa taka za kielekroniki katika miji na manispaa, changamoto na fursa zilizopo katika taka za kielektroniki,  Udhibiti wa madampo haramu, Mpango mkakati wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira, Mchakato wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii pamoja na Kaguzi za Mazingira pamoja na mchakato wa kupata vibali vya taka hatarishi pamoja na changamoto zilizopo katika udhibiti wake. 


Baadhi ya maafisa wa NEMC wakiwasilisha mada katika Mafunzo hiyo

Katika kuhitimisha mafunzo hayo baadhi ya washiriki wamelishukuru Baraza kwa mafunzo hayo huku wakieleza kuwa wamepata mbinu mpya ambazo awali hawakuwa nazo katika swala zima la Usimamizi wa Mazingira nchini.



Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo

NEMC YAZITAKA TAASISI ZA UMMA KUTEKELEZA KWA UFANISI SHERIA YA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limezitaka taasisi za umma zikiwemo Wizara, Idara, Wakala wa Serikali na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake yanatekelezwa ipasavyo katika maeneo yao ya kazi.

Wito huo umetolewa leo, tarehe 20 Agosti 2025, katika semina ya mafunzo ya nyenzo za usimamizi wa mazingira chini ya Mradi wa EMA kwa Taasisi za Umma inayoendelea katika Hoteli ya Midland, Jijini Dodoma kuanzia tarehe 20 hadi 21 Agosti 2025.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, mgeni rasmi ambaye ni Meneja wa Maeneo Maalumu na Mabadiliko ya Tabianchi, Dkt. Careen Anatory Kahangwa, amesema lengo la semina hiyo ni kuimarisha mbinu za kazi na uwezo wa utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, sambamba na kuimarisha mifumo ya kisheria na kitaasisi kwa ajili ya usimamizi bora wa mazingira nchini.

Meneja wa Maeneo Maalumu na Mabadiliko ya Tabianchi (NEMC), Dkt. Careen Anatory Kahangwa akizungumza wakati wa Semina ya kujenga uwezo wa kitaifa juu ya nyenzo za Usimamizi wa Mazingira nchini kwa Wizara, Taasisi na Mamlaka za Serikali za Mitaa chini ya Mradi wa EMA.

"Ushiriki wenu katika kikao hiki ni wa muhimu kwa kuwa unalenga kuhakikisha utekelezaji wa sheria za kitaifa na mikataba ya kimataifa ya mazingira. Hii itawezekana tu iwapo mtayapokea mafunzo haya kwa umakini na kuyazingatia ili kujengewa uwezo wa kutosha katika kusimamia vyema mazingira," alisema Dkt. Kahangwa.

Kwa upande wake, Afisa Mazingira Mkuu wa NEMC na Mratibu Mkuu wa Mradi wa EMA, Bw. Paul Mashaija Kalokola ameeleza kuwa kumekuwa na uhitaji mkubwa wa kujengea uwezo taasisi mbalimbali ili wadau waweze kufahamu na kutumia nyenzo muhimu za usimamizi wa mazingira nchini.

Afisa Mazingira Mkuu wa NEMC na Mratibu Mkuu wa Mradi wa EMA upande wa NEMC, Bw. Paul Mashaija Kalokola akizungumza katika Semina hiyo

Ameongeza kuwa changamoto kubwa kwa sasa ni udhaifu wa baadhi ya taasisi katika kutekeleza ipasavyo Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, hali iliyosababisha kuanzishwa kwa mradi huo wa miaka mitatu unaosimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais, wenye lengo la kuimarisha uwezo wa wadau wote nchini katika kusimamia mazingira kwa ufanisi.

Baadhi ya washiriki wa semina ya mafunzo ya nyenzo za usimamizi wa mazingira chini ya Mradi wa EMA   





Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo wakichangia mada 


Washiriki wa Semina  ya kujenga uwezo kitaifa juu ya nyenzo za usimamizi wa Mazingira chini ya Mradi wa EMA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya awamu ya kwanza ya mafunzo hayo


NEMC YAWATAKA WAMILIKI WA MABASI KUIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA BARABARANI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limewataka wamiliki wa vyombo vya usafiri pamoja na abiria kuboresha usafi katika mabasi na maeneo ya usafiri barabarani, kwa kuzuia tabia ya kutupa taka nje ya magari na kukojoa mabarabarani.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi alipokuwa akiongea na vyombo vya habari kuhusu umuhimu wa kuhifadhi na kusimamia Mazingira nchini. 

Amesema kumekuwepo na mitazamo iliyojengeka kwa abiria wa mabasi makubwa yanayoenda safari ndefu na fupi ya kutokuthamini mazingira na kuwa na tabia ya kutupa taka ovyo na kukojoa barabarani hali inayochafua mazingira, kuharibu hali ya hewa na kuhatarisha afya za jamii. 

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akizungumza na vyombo vya Habari wakati akitoa wito wa kuwataka wamiliki wa vyombo vya usafiri kuepuka uchafuzi wa mazingira.

“Mazingira safi ni haki ya kila Mtanzania, na ni jukumu letu sote kuhakikisha tunayahifadhi. Kutupa taka nje ya gari na kukojoa barabarani si tu ni tabia mbaya, bali pia ni ukiukwaji wa Sheria za mazingira. Tunawaomba wasafiri na wamiliki wa mabasi kushirikiana nasi kwa kuweka na kutumia vyombo vya kutupa taka ili tukome uchafuzi huu,” alisema Mkurugenzi Mkuu Dkt. Immaculate Sware Semesi

Aidha, NEMC imetahadharisha kuwa watakaobainika kutupa taka au kukojoa mabarabarani watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo faini na adhabu nyingine zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria za mazingira.

“Ninawahimiza watanzania wote kuwa mabalozi wa usafi katika maeneo wanayopitia. Tukichukua hatua sasa, tunaweza kulinda afya zetu na mazingira kwa vizazi vya sasa na baadae”.

NEMC imeendelea kutoa simu ya bure 0800 110 115 kwa ajili ya kuripoti uchafuzi wa Mazingira unaosababishwa na abiria, shughuli za binadamu, viwanda bubu au raia ili kuimarisha usimamizi na kuleta mabadiliko chanya katika jamii

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA KAMATI YA KIMATAIFA GENEVA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC limeshiriki Mkutano wa kamati ya kimataifa ya majadiliano ya kuanzisha mkataba wa kimataifa wa kukabiliana na uchafuzi unaotokana na Plastiki nchini nchini Uswisi mjini Geneva

Mkutano huo umehusisha jopo la wadau wa Mazingira kutoka nchini Tanzania likiongozwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) profesa Peter Msofe, Balozi wa Tanzania nchini Kenya, maafisa kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, NEMC, TBS, na GCLA ambao walishiriki kikamilifu kwa siku zote kumi za majadiliano ya kuanzishwa Mkataba huo.

Meneja wa Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bw. Hamadi Taimuru akiwasilisha mada katika Mkutano huo

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msoffe (wa kwanza kulia) na Bw. Hamadi Taimuru (wa pili kushoto) wakifuatilia Mkutano huo


Hata hivyo kutokana na mitazamo na misimamo ya nchi mbalimbali kulingana na maslahi ya nchi zao, majadiliano hayo hayakuweza kufikia muafaka na hivyo mwenyekiti wa Mkutano ndugu Luisaliaghirisha majadiliano mpaka pale atakapotangaza tarehe mpya ya kuendeleza majadiliano hayo na hatimaye kupata mkataba husika.

Majadiliano ya washiriki wa Mkutano huo ikiwa ni sehemu ya Mkutano huo

NEMC YAUNGANA NA TAASISI NYINGINE KUADHIMISHA SIKU MAALUMU YA MAZINGIRA MAONESHO YA SABASABA 2025

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC  Julai 6, 2025  limeungana na Taasisi mbalimbali kuadhimisha Siku ya maalumu ya Mazingira iliyotengwa kwa mara ya kwanza kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba) 2025.

Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo alikuwa ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhandisi Cyprian Luhemeja huku tukio hilo likibebwa na Kauli mbiu isemayo "Matumizi ya Nishati safi na utunzaji wa Mazingira Kwa ustawi wa Tanzania bora".


Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza wakati wa hafla ya Siku maalumu ya Mazingira iliyotengwa katika maonesho ya Sabasaba 2025 iliyofanyika tarehe 6/7/2025

Akizungumza katika hotuba yake Mhe. Cyprian Luhemeja ameitaka siku hiyo ya tarehe 6 /7 itengwe rasmi kuwa siku maalumu ya Mazingira kila mwaka katika maonesho hayo kuanzia maonesho ya 50 ya biashara ya kimataifa (sabasaba).

Hafla ya Siku maalum ya Mazingira tarehe 6/7/2025 iliyotengwa katika msimu wa maonesho ya Sabasaba 2025

Sambamba na hilo amesisitiza watanzania wote kutunza Mazingira kwa kuwa Mazingira yaliumbwa kwanza Kisha mwanadamu akaumbwa baadae ili ayatunze, ayahifadhi na kuyalinda.

"Hii duniani ilianza kwa kutengenezewa Mazingira, mwanadamu ameumbwa wa mwisho baada ya Mazingira kutengenezewa na mwanadamu alipoumbwa alipewa kazi ya kuyatunza na kuyahifadhi Mazingira lakini mwanadamu anayaharibu kwa uchafuzi na ukataji wa miti.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC Bi. Mwanasha Tumbo (wa pili kulia) Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi (wa tatu kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa  Tantrade, Dkt. Latifa M. Khamis (wa tatu kulia), timu ya wanawake na Samia na baadhi ya washiriki wa Siku maalumu ya Mazingira iliyotengwa katika msimu wa maonesho ya Sabasaba 2025

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza Dkt. Immaculate Sware Semesi amewapongeza washindi wa Mazingira Challenge iliyofanyika siku kadhaa zilizopita ambayo ililenga kumpata balozi kinara wa  Utunzaji wa Mazingira na anayehamasisha utunzaji wa Mazingira kwa kupiga picha ya Mazingira safi yanayomzunguka na kuwasilisha NEMC Kwa ajili ya mashindano hayo.

Maadhimisho hayo yalipambwa na mabalozi wa Mazingira pamoja na watumbuizaji nguli akiwemo Mrisho Mpoto pamoja na Mr. Tree na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Menejimenti ya NEMC, TANTRADE, STAMICO, Wanawake na Samia, Shirika la PUMA pamoja na wananchi waliotembelea maonesho ya sabasaba.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akimkabidhi zawadi na cheti cha heshima Mshindi wa kwanza wa mashindano ya ‘Mazingira Challenge’ Bw. Paulo Dotto Masele yaliyofanyika katika msimu wa sabasaba

Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akimkabidhi zawadi na cheti cha heshima Mshindi wa pili wa mashindano ya ‘Mazingira Challenge’ Bi. Magdalena Chuma yaliyofanyika katika msimu wa sabasaba


Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja akimkabidhi zawadi na cheti cha heshima Mshindi wa tatu wa mashindano ya ‘Mazingira Challenge’ Bw. Stanley Urassa  yaliyofanyika katika msimu wa sabasaba

"Hii duniani ilianza kwa kutengenezewa Mazingira, mwanadamu ameumbwa wa mwisho baada ya Mazingira kutengenezewa na mwanadamu alipoumbwa alipewa kazi ya kuyatunza na kuyahifadhi Mazingira lakini mwanadamu anayaharibu kwa uchafuzi na ukataji wa miti.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza Dkt. Immaculate Sware Semesi amewapongeza washindi wa Mazingira Challenge iliyofanyika siku kadhaa zilizopita ambayo ililenga kumpata balozi kinara wa  Utunzaji wa Mazingira na anayehamasisha utunzaji wa Mazingira kwa kupiga picha ya Mazingira safi yanayomzunguka na kuwasilisha NEMC Kwa ajili ya mashindano hayo.

Maadhimisho hayo yalipambwa na mabalozi wa Mazingira pamoja na watumbuizaji nguli akiwemo Mrisho Mpoto pamoja na Mr. Tree na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Menejimenti ya NEMC, TANTRADE, STAMICO, Wanawake na Samia, Shirika la PUMA pamoja na wananchi waliotembelea maonesho ya sabasaba.



Ugawaji wa Zawadi kwa Wadau wengine 


NEMC YAPIGA KAMBI SABASABA – YAWAKARIBISHA WANANCHI KUPATA ELIMU YA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) lilipiga kambi viwanja vya sabasaba maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ili kutoa elimu ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa wananchi waliotembelea banda hilo katika Jengo la Karume.

Akizungumza katika maonesho hayo, Mhandisi Mwandamizi wa NEMC, Bw. Haji Kiselu, alisema Baraza limejipanga kikamilifu kuhakikisha elimu ya mazingira iliyo jumuishi inamfikia kila mwananchi, ili kwa pamoja tuweze kuyasimamia kwa maendeleo endelevu nchini.

Kwa upande wake, Mhandisi wa NEMC, Bw. Peres Ntinginya, alipozungumza, alisisitiza kuwa utunzaji wa mazingira ni jukumu la kila mmoja hivyo yapasa kuwajibika na kutoa  wito kwa wananchi kutumia nishati safi ya kupikia kwa kuwa matumizi yake husaidia kulinda afya ya binadamu na viumbe hai, kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa, pamoja na kuhifadhi mazingira kwa ujumla.

Naye Mkazi wa Rufiji, Bw. Ayubu Njanja, alisema elimu aliyoipata kutoka kwa Maafisa wa Baraza imempa mwongozo sahihi wa kuzingatia katika kuhakikisha 

Bw. Ayubu Njanja akipatiwa elimu ya mazingira kutoka kwa wataalam wakati wa msimu wa maonesho ya 49 ya Sabasaba. 




Elimu ya Mazingira ikitolewa kwa wageni waliotembelea banda la NEMC katika  maonesho ya 49 ya Sabasaba 2025 




Elimu ya Mazingira ikitolewa kwa wageni waliotembelea banda la NEMC katika  maonesho ya 49 ya Sabasaba 2025 


NEMC YATEKELEZA AGIZO LA RAIS, YAONGEZA HUDUMA VIWANJA VYA NZUGUNI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetekeleza agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan la kuongeza muda wa kutoa huduma zake katika viwanja vya maonesho ya Nane Nane vilivyopo Nzuguni, Jijini Dodoma. 

Hatua hiyo inalenga kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi, hususan wakulima na wafugaji wanaoshiriki maonesho hayo, ili kuwajengea uelewa na kuwasaidia kutekeleza shughuli zao kwa kuzingatia utunzaji wa mazingira.

Elimu ya Mazingira ikitolewa kwa wageni waliotembelea banda la NEMC katika maoneshoya wakulima, Nanenane 2025 katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma katika siku za nyongeza ikiwa ni agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuongeza muda wa maonesho hayo

NEMC inaendelea kutoa elimu inayohusu masuala ya matumizi endelevu ya ardhi, uhifadhi wa vyanzo vya maji, na namna ya kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi katika sekta ya kilimo na ufugaji.

Vilevile, wananchi wameelimishwa kuhusu taratibu za kupata vibali vya mazingira na umuhimu wa kufanya Tathmini ya athari kwa mazingira kabla ya kuanzisha miradi.

Baraza hilo linaendelea kuwakaribisha wananchi wote kutembelea banda lake ili kushirikiana kwa pamoja katika kusimamia na kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu ya Taifa. 

“Mazingira ni msingi wa maisha yetu. Tukiyaacha, na sisi tutapotea. Tushirikiane kuyatunza kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo,”



Elimu ya Mazingira ikitolewa kwa wageni waliotembelea banda la NEMC katika maonesho ya wakulima, Nanenane 2025 katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma katika siku za nyongeza ikiwa ni agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuongeza muda wa maonesho hayo


NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...