Nyumbani

RUVUMA YAFIKIWA ELIMU YA MAZINGIRA- MADINI YA URANIUM

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) lilitoa elimu ya kimazingira na afya kwa vijiji viwili vya Mtonya na Mandela-Likuyu katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma kufuatia Mradi wa Uchimbaji wa Madini aina ya 'Uranium'  ulitarajiwa kuanza katika mgodi ulio karibu na vijiji hivyo.

Elimu hiyo ilitolewa kwa wananchi kuanzia 8-9 Septemba, 2025 kwa vijiji hivyo huku ikifuatiwa na ukaguzi uliofanyika katika mgodi huo ambapo ilikuwa hatua ya awali ya kuelimisha jamii na wawekezaji kabla ya Mradi huo kuanza ambapo  ni maagizo yaliyotolewa na Serikali ili kuhakikisha jamii inatambua uwepo wa Mradi huo na kuhakikisha  jamii haiathiriki na Mradi huo.

Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti akizungumza wakati wa utoaji wa elimu ya ya Mazingira na Afya kwa wanakijiji wa Mtonya Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma kufuatia Uchimbaji mkubwa wa madini ya 'Urunium' utakaoanza mwakani 2026

Meneja Kanda ya Kusini NEMC Bw. Boniface Guni akiwasilisha mada kwa wanakijiji wa Mandela-Likuyu Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma wakati wa utoaji wa elimu ya Mazingira na Afya kufuatia Uchimbaji mkubwa wa madini ya 'Urunium' utakaoanza mwakani 2026

Meneja Kanda ya Kusini NEMC Bw. Boniface Guni akiwasilisha mada kwa wanakijiji wa Mtonya Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma wakati wa utoaji wa elimu ya Mazingira na Afya kufuatia Uchimbaji mkubwa wa madini ya 'Urunium' utakaoanza mwakani 2026

Akizungumza katika utoaji wa elimu hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi, Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti aliutaka Uongozi wa vijiji hivyo kutumia Kamati za Mazingira na kushirikiana na Serikali kuendelea kuelimisha jamii juu ya maswala ya Mazingira na Afya ya jamii yanayoweza kusababishwa na Mradi huo.

Kwa upande wake, Meneja Kanda ya Kusini (NEMC) Bw. Boniface Guni aliwataka wakazi wa vijiji hivyo kuchangamkia fursa za ajira katika Mradi huo huku wakizingatia ulinzi wa Afya zao na Mazingira.

Aidha Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria NEMC Bw. Jamal Baruti alisema NEMC itaendelea na ufuatiliaji wa maswala ya kimazingira kwa kushirikiana na Taasisi nyingine huku akiitaka Kampuni ya Mantra TZ LTD ya Uchimbaji katika mgodi huo kutambua haki za wakazi wa vijiji hivyo na kuchangia shughuli za maendeleo ya wakazi wa vijiji hivyo kama manufaa ya Mradi huo.

Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti (wa tatu kulia waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanakijiji na Viongozi wa Kijiji cha Mtonya Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma mara baada ya kuwapatia elimu ya Mazingira na Afya kufuatia Uchimbaji mkubwa wa madini ya 'Urunium' utakaoanza mwakani 2026

NEMC YASHIRIKI MAONESHO YA KIMATAIFA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KUSINI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara na Uwekezaji Kusini (Kusini International Trade Fair and Festival) yanayofanyika kuanzia tarehe 14-21, Septemba, 2025 katika eneo la fukwe ya Matema Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya.

Maonesho hayo yamelenga kutangaza fursa za kibiashara zilizopo katika mikoa ya Kusini ambapo NEMC inatumia fursa hiyo kutoa elimu ya Mazingira.


Maafisa Mazingira wa NEMC Kanda ya Kusini wakitoa elimu kwa wananchi waliotembelea banda lao katika maonesho hayo.

DKT. SERERA AVUTIWA NA USHIRIKI WA NEMC KWENYE MAONESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA BARANI AFRIKA (IATE)

Naibu Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera amelipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa namna ambavyo linatoa elimu kwa wadau mbalimbali wakiwemo wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Barani Afrika yanayotambulika kama Intra African Trade Fair (IATF) yanayoendelea jijini Algiers nchini Algeria kuanzia Septemba 4-10, 2025.

Dkt. Serera ambaye ni Mkuu wa msafara wa Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Maonesho hayo, ametoa pongezi hizo alipofika Banda la Tanzania akiambatana na mwenyeji wake ambaye ni Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Iman S. Njalikai.

Naibu Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera akizungumza na Mhandisi Mwandamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Peres Ntiginya wakati alipotembelea Banda la Tanzania katika maonesho hayo

"Uchumi tunaoutaja ni Uchumi wa Viwanda, lakini Viwanda tunavyohitaji ni viwanda vinavyozingatia Uhifadhi wa Mazingira, hivyo basi NEMC kwa kuja hapa wanawaambia wawekezaji waje lakini yapo ya kuzingatia kuhusu Utunzaji na Uhifadhi wa Mazingira" amesema Dkt. Serera.

"NEMC inalo jukumu la kuendelea kutoa elimu na nilichopenda zaidi ni kwamba hakuna urasimu, nimeona hapa taarifa zote unaweza kuzisoma na kuzipata kupitia "QR Code" kabla hata ya kuja kuwekeza Tanzania, Na hapa niwapongeze sana NEMC kwa namna mnavyofanya kazi vizuri na muendelee hivyo kwani Mazingira ni uhai ni lazima tuyatunze ili yatutunze" Amesisitiza Dkt. Serera.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Imani S. Njalikai amezitaka Taasisi zinazoshiriki Maonesho hayo kuitumia fursa hii vizuri hasa katika maeneo ambayo Algeria inafanya vizuri kwenye sekta ya nishati ambayo ni pamoja na gesi, mafuta, mbolea na sekta ya madawa (pharmaceutical) ambayo ni pamoja na mafunzo kwenye maeneo hayo.

Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara, Dkt. Suleiman Serera katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Barani Afrika yanayotambulika kama Intra African Trade Fair (IATF) yaliyofanyika jijini Algiers nchini Algeria kuanzia Septemba 4-10, 2025.

NEMC ikiwa ni moja ya Taasisi inayoshiriki Maonesho hayo ikiwakilishwa na Mhandisi Mkuu, Peres Ntinginya na Afisa Uhusiano na Mawasiliano, Bw. Tajiri Kihemba. Taasisi nyingine zinazoshiriki ni pamoja na TANTRADE ambao ni waratibu kwa upande wa Tanzania, TMDA, FCC, TISEZA, PURA, TFS, ZIPA.

NEMC YASHIRIKIANA NA ASASI ZA KIRAIA KUSAFISHA FUKWE YA COCO, ΝΙΚΑΤΙΚΑ KUTΕΚELEΖΑ ΚΑΜΡENI YA ΝΕΜC USAFI KAMPENI'

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC, Asasi za kiraia na wakazi wa karibu na maeneo ya fukwe ya Coco leo 6 Septemba, 2025 wamefanya usafi wa fukwe ya Coco ikiwa ni sehemu ya Utekelezaji wa Kampeni ya 'NEMC Usafi Kampeni' iliyozinduliwa rasmi 4 Septemba, 2025.

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Mhandisi wa Mazingira (NEMC) Bw. Joshua Muro amesema NEMC ipo tayari kushirikiana na jamii pamoja na Asasi za kiraia katika kutekeleza Kampeni hiyo ya 'NEMC Usafi Kampeni' yenye lengo la kuhamasisha jamii kusafisha na kuhifadhi Mazingira, Pia ameitaka jamii kubadili mtazamo juu ya jukumu la usafi wa Mazingira na kufafanua kuwa ni jukumu la kila mmoja kufanya usafi wa Mazingira yanayomzunguka.

Baadhi ya watumishi wa NEMC na DEPO wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya zoezi la usafi katika Fukwe ya Coco

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Asasi ya DEPO, Ndugu. Humphrey Milinga amesema lengo kubwa la zoezi hilo ni kuhamasisha jamii katika ngazi ya familia kusafisha Mazingira na kujumuika katika vikundi vya usafishaji Mazingira zikiwemo Fukwe.

Washiriki wengine walio jumuika katika zoezi hilo ni Africraft, MBC, WWF, TIA, TESCAR na Bethlehem Parish.

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira linaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa Mazingira na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Asasi za kiraia pamoja na wadau wengine ili kuhakikisha nchi yetu inakuwa na safi na salama kwa ustawi wa Afya na Mazingira.

Baadhi ya wakazi wa maeneo ya jirani na Fukwe ya Coco na baadhi ya watumishi wa NEMC kisafisha Fukwe hiyo


NEMC YAJA NA USAFI KAMPENI 2025

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limezindua kampeni mpya ya usafi iitwayo "NEMC Usafi Kampeni' 2025" yenye lengo la kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika usafi wa mazingira na kuhakikisha nchi inakuwa safi, salama na yenye afya kwa wote.

Kampeni hiyo ambayo itatekelezwa kwa ushirikiano na Ofisi ya Rais - TAMISEMI, mamlaka za mikoa na Halmashauri, Taasisi binafsi, Asasi zisizo za kiserikali na wananchi, inalenga kuibua mabadiliko ya tabia na kukuza uwajibikaji wa pamoja katika kudhibiti ongezeko la uchafuzi wa mazingira, hasa taka ngumu na plastiki.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na utekelezajinwa Sheria NEMC Bw. Jamal Baruti, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu alisema kwa sasa Tanzania inazalisha takriban tani milioni 14.4 hadi 20.7 za taka kwa mwaka, huku wastani wa uzalishaji taka kwa mtu mmoja ukiwa kati ya kilo 0.66 hadi 0.95 kwa siku. Hali hii inahitaji jitihada za dhati kutoka kwa kila mtanzania.

"Kampeni hii inalenga kuondoa dhana kuwa usafi ni jukumu la serikali pekee. Kila mtu anapaswa kushiriki, kwa kuwa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 inamtaka kila mtu kuwa mdau na mlinzi wa mazingira," alisema Baruti.

Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti akizungumza na Vyombo vya habari katika Uzinduzi wa Kampeni hiyo

Aliongeza kuwa kampeni hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050, ambayo imeweka hifadhi ya mazingira kuwa moja ya mihimili ya maendeleo endelevu. Kupitia kampeni hii, taka zitatazamwa kama fursa ya ajira kupitia miradi ya kijani, vijana na wanawake watawezeshwa kupitia mafunzo ya ujasiriamali wa mazingira, huku upandaji miti ukihamasishwa kwa nguvu zote.

Miongoni mwa shughuli zitakazofanyika chini ya kampeni hiyo ni pamoja na operesheni za usafi, mafunzo ya elimu ya mazingira, mashindano ya usafi kwa shule na kata, uanzishaji wa bustani za kijani, maonesho ya bidhaa rafiki kwa mazingira, pamoja na uanzishwaji wa klabu za mazingira katika shule zote za msingi na sekondari ifikapo Juni 2026.

Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na utekelezajinwa Sheria (NEMC) Bw. Jamal Baruti akizungumza na Vyombo vya habari katika Uzinduzi wa Kampeni hiyo

Meneja wa Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bw. Hamad Taimuru (kushoto) akielezea jambo wakati  wa uzinduzi wa "NEMC Usafi Kampeni"..

NEMC YAWANOA MAWAKILI WA SERIKALI SHERIA YA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa mafunzo ya uelewa wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira na utekelezaji wa majukumu yake kwa mawakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.

Akizungumza katika Mafunzo hayo tarehe 3 Septemba, 2025 Mkurungenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Semesi amesema kuwa wameandaa mafunzo hayo kwa lengo la kujengeana uelewa wa kisheria katika usimamizi wa mazingira nchini pamoja na kuboresha mahusiano mazuri katika Usimamizi na Utekelezaji wa Sheria za Mazingira nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akizungumza katika Mafunzo hayo 

Akifungua Mafunzo hayo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amesema wanasheria hao wanatakiwa kuwa walinzi na kuongeza umakini katika kutoa ushauri wa sheria za mazingira kwa maslahi ya nchi.

"Natambua zipo changamoto wakati wa utekelezaji, mfano uelewa mdogo wa masuala ya mazingira hivyo tunawajibu wa kuzibadili changamoto hizi na kuzifanya fursa kwa kuimarisha nafasi ya NEMC katika kusimamia sheria katika sekta ya mazingira."Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali amelishukuru Baraza na kueleza kuwa mafunzo hayo yataongeza uelewa kwa Mawakili wa Serikali hivyo kuwasaidia wakati watakapokuwa wanatoa Ushauri wa Kisheria na Upekuzi wa Mikataba inayohusu hifadhi na usimamizi wa mazingira nchini.

Baadhi ya Mawakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria wakifuatilia mafunzo hayo

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari akieleza jambo wakati wa Mafunzo hayo
Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akimweleza jambo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari mara baada ya Mafunzo hayo, Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Utawala na Fedha (NEMC) Bw. Dickson Mjinja na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Sheria NEMC, Bw. Joannes Karungura 

Picha ya pamoja mara baada ya mafunzo hayo

NEMC YAJENGEWA UWEZO KUPITIA MAFUNZO YA KIMATAIFA KUHUSU UFADHILI WA MIRADI YA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na African Adaptation Initiative (AAI), limeandaa warsha ya siku tatu kwa ajili ya kuwajengea uwezo wataalamu wake kuhusu mbinu bora za kupata na kusimamia fedha za miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambayo inafanyika kuanzia 26-28 Agosti, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa NEMC.

AAl, ambayo ilianzishwa na Wakuu wa Nchi za Afrika, inalenga kusaidia mataifa ya Bara la Afrika katika kuongeza uwezo wao wa kupata rasilimali za kifedha za kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.


Baadhi ya wajumbe kutoka  African Adaptation Initiative (AAI) wakiwasilisha mada katika Warsha hiyo

Kupitia mpango wake mahsusi uitwao Adaptation Project Incubator for Africa (APIA), AAl inasaidia taasisi na nchi wanachama kuboresha uandishi, uandaaji na utekelezaji wa miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Aidha, NEMC iliingia makubaliano ya ushirikiano (MoU) na AAl ili kuwezesha Tanzania kunufaika na fursa hii ya mafunzo. Warsha hii ni matokeo ya makubaliano hayo na inalenga kuimarisha uelewa wa wataalamu wa NEMC katika maeneo mbalimbali ikiwemo: Mifumo ya kitaasisi na kifedha kuhusu mabadiliko ya tabianchi, Uandishi na uwasilishaji wa Miradi ya kimataifa, Usimamizi wa utekelezaji wa miradi, na mbinu za kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya kimataifa kuhusu fedha za miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.


Watumishi wa Baraza wakichangia mada katika Warsha hiyo

Baadhi ya Watumishi wa Baraza wakifuatilia mafunzo ya Warsha hiyo





Picha ya pamoja mara baada ya kuhitimishwa kwa Warsha ya siku tatu yakuwajengea uwezo wataalamu wa NEMC kuhusu mbinu bora za kupata na kusimamia fedha za miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi iliyofanyika kuanzia 26-28 Agosti, 2025 

Kupitia mpango wake mahsusi uitwao Adaptation Project Incubator for Africa (APIA), AAl inasaidia taasisi na nchi wanachama kuboresha uandishi, uandaaji na utekelezaji wa miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Aidha, NEMC iliingia makubaliano ya ushirikiano (MoU) na AAl ili kuwezesha Tanzania kunufaika na fursa hii ya mafunzo. Warsha hii ni matokeo ya makubaliano hayo na inalenga kuimarisha uelewa wa wataalamu wa NEMC katika maeneo mbalimbali ikiwemo: Mifumo ya kitaasisi na kifedha kuhusu mabadiliko ya tabianchi, Uandishi na uwasilishaji wa Miradi ya kimataifa, Usimamizi wa utekelezaji wa miradi, na mbinu za kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya kimataifa kuhusu fedha za miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Kupitia mafunzo haya, NEMC inatarajiwa kuongeza uwezo wake wa kuandaa na kusimamia miradi mikubwa ya kimkakati, hivyo kuisaidia Tanzania kuongeza fursa za kupata fedha za kimataifa kwa ajili ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...