Ziara hii imelenga kuimarisha ushirikiano katika udhibiti wa uchafuzi, taarifa za mabadiliko ya tabianchi na maendeleo yenye uzalishaji mdogo wa hewa chafuzi.
Kupitia mpango wa Nishati kwa Maendeleo (Energy for Development - EfD), NEA inashirikiana na nchi za Afrika zikiwemo Tanzania, Nigeria, Msumbiji, Malawi, Uganda, Ghana na Afrika Kusini. Ushirikiano wa sasa kati ya Tanzania na Norway unalenga udhibiti wa uchafuzi wa mazingira na utoaji wa taarifa za hali ya hewa, lakini unaweza kuongezwa baada ya mwaka 2026 kujumuisha maeneo mapana zaidi kama mabadiliko ya tabianchi, bayoanuai na usimamizi wa uchafuzi
Mamlaka ya Mazingira ya Norway (Norwegian Environment Agency - NEA) ndiyo taasisi kuu inayotekeleza sera za mazingira za Norway chini ya Wizara ya Hali ya Hewa na Mazingira. Muundo wake wa uongozi ni rahisi, Serikali, Wizara, NEA, Magavana na Halmashauri za Manispaa na inatoa ushauri kuhusu mabadiliko ya tabianchi, bayoanuai, uchafuzi wa mazingira na matumizi ya ardhi. NEA pia huandaa Ripoti za Hali ya Mazingira, hutoa kanuni na vibali, na kushirikiana kitaifa na kimataifa.
Mfumo wa kisheria wa Norway wa udhibiti wa hewa chafu unajumuisha Sheria ya Udhibiti wa Uchafuzi (Pollution Control Act, 1993), Usalama na Mazingira (HSE) kwa shughuli za mafuta na gesi, Kanuni za Uchafuzi na Taka, Vibali vya Udhibiti wa Uchafuzi, Sheria ya Biashara ya Uzalishaji wa Gesi Joto (Greenhouse Gas Emissions Trading Act), na Sheria ya Ulinzi wa Uanuai (Nature Diversity Act). Sheria hizi huipa NEA mamlaka ya kudhibiti utoaji wa gesi chafuzi kama methane na kabonidaioksaidi (CO2) na kuhakikisha ufuatiliaji na utekelezaji wa masharti kwa sekta mbalimbali, zikiwemo mafuta na taka.
Kwa kadirio la uzalishaji wa methane kutoka dampo na maeneo ya utupaji taka, NEA hutumia mbinu za Shirika la Kiserika