Nyumbani

NEMC NA ZEMA ZAKUBALIANA KATIKA USIMAMIZI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA NCHINI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) wameimarisha ushirikiano wao kuingia  makubaliano ya pamoja ya usimamizi na uhifadhi wa mazingira nchini. 

Makubaliano hayo yamefikiwa katika kikao cha siku mbili kilichofanyika kuanzia tarehe 7 hadi 8 Oktoba 2025, ambapo wajumbe wa Bodi na wataalamu kutoka taasisi zote mbili walikutana kujadiliana na kubadilishana uzoefu kuhusu utekelezaji wa majukumu yao.

Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa kikao hicho

Kupitia kikao hicho, taasisi hizo zimeweka msingi wa ushirikiano madhubuti katika maeneo mbalimbali, yakiwemo matumizi ya teknolojia ya kidijitali katika usimamizi wa mazingira, ufuatiliaji wa utekelezaji wa sheria na Kanuni za mazingira, pamoja na kuimarisha mawasiliano ya mara kwa mara kati ya pande hizo mbili.

Aidha  wamekubaliana pia kuhakikisha kuwa miradi yote inayotekelezwa upande wa Tanzania Bara na Zanzibar inazingatia mchakato wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA).

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akizungumza wakati wa Kikao hichoMwenyekiti wa Bodi ya ZEMA Bi. Asha Ali Khatib akizungumza wakati wa Kikao hicho

Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya NEMC na ZEMA wakifuatilia kikao hicho

Akizungumza na vyombo vya habari, Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Mhandisi Mwanasha Tumbo, amesema ushirikiano huo ni hatua muhimu kuelekea utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2020/2050, ambayo inaweka mazingira kama mojawapo ya nguzo kuu za maendeleo ya Taifa.

 Amesisitiza kuwa mashirikiano hayo yataongeza ufanisi katika utendaji kazi na kusaidia kufanikisha malengo ya kitaifa ya uhifadhi wa mazingira kwa maslahi ya wananchi na vizazi vijavyo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya ZEMA, Bi. Asha Ali Khatib, amesema kikao hicho kimetoa fursa kwa wataalamu wa pande zote mbili kujifunza kutoka kwa wenzao, na pia kuibua mbinu mpya za kuboresha utendaji.

Ameongeza kuwa ushirikiano huu utawezesha uwiano wa kisera na kiutekelezaji katika masuala ya mazingira baina ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Picha ya pamoja ya Menejimenti ya NEMC na ZEMA mara baada ya Kikao hicho. Wa nne kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Mhandisi Mwanasha Tumbo, kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya ZEMA Bi. Asha Ali Khatib, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa ZEMA Sheha Mjaja Juma


NEMC NA ZEMA ZAIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA UHIFADHI NA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) leo Oktoba 7,2025 limepokea ugeni wa Menejimenti ya Mamlaka ya Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) na kufanya kikao Cha kujengeana uwezo ikiwa ni mwendelezo wa juhudi za kuimarisha ushirikiano katika kusimamia na kuhifadhi mazingira nchini

Akifafanua lengo la kikao hicho Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi amesema kimejikita katika kujadiliana mikakati, kutoa ushauri na kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli za mazingira kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hizo na kuongeza tija katika sekta ya mazingira.

Pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi (Kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa ZEMA Bw. Sheha Mjaja Juma mara baada ya kikao cha kujengeana uwezo kati ya Taasisi hizo mbili

Viongozi hao pia wamejadili utekelezaji wa taratibu walizojiwekea katika kufuatilia na kusimamia Sheria za mazingira ili kuhakikisha rasilimali asilia zinatunzwa ipasavyo kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa ZEMA, Bw. Sheha Mjaja Juma amesisitiza umuhimu wa wananchi kutimiza wajibu wao kwa kufuata Sheria na taratibu za mazingira, sambamba na Taasisi za maendeleo kuhakikisha miradi yao inazingatia usimamizi endelevu wa mazingira ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi.

Itakumbukwa kuwa NEMC na ZEMA wamekuwa na mashirikiano ya muda mrefu na mara kadhaa wamekuwa wakitembeleana na kupeana uzoefu kwa maslahi mapana ya Mazingira nchini Tanzania.

Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya NEMC na ZEMA wakifuatilia kikao hicho
Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akizungumza na vyombo vya Habari mara baada ya Kikao hicho
Mkurugenzi Mkuu wa ZEMA Bw. Sheha Mjaja Juma  akizungumza na vyombo vya Habari mara baada ya Kikao hicho



NEMC YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA MTEJA KWA VITENDO

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa mteja yenye kaulimbiu " Mission Possible" limeweka banda maalum katika ofisi zake ili kurahisisha  huduma kwa wateja wake moja kwa moja. 

Banda hilo limelenga kuboresha mawasiliano na kujenga mahusiano bora yenye kutoa fursa kwa wadau  kutoa maoni, changamoto, pamoja na kupatiwa majibu ya papo kwa papo kuhusu huduma za mazingira.

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi akiwa katika banda maalum la kuhudumia wateja lililopo Ofisi za NEMC katika msimu wa Wiki ya Huduma kwa Mteja inayoadhimishwa kuanzia tarehe 6 hadi 10 Oktoba, 2025  

Wateja waliofika Ofisi za NEMC wakipatiwa huduma katika Wiki ya Huduma kwa Mteja 
Mkurugenzi wa Utawala na Fedha (NEMC) Bw. Dickson Mjinja akifuatilia utoaji wa huduma kwa wateja waliofika katika banda maalum la NEMC katika Maadhimisho ya Wiki ya huduma kwa Mteja 

Katika hatua nyingine Baraza Kupitia Kanda zake 13  limeendelea kutoa elimu ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira kwa wanachi

Ikiwa ni pamoja na kufanya ziara za ukaguzi (site visits) kwa wadau wake kujiridhisha na utekelezaji wa Kanuni za mazingira na kushughulikia changamoto zinazoibuliwa na wananchi


WATAALAM ELEKEZI WA MAZINGIRA KANDA YA MAGHARIBI (NEMC) WAPATIWA MAFUNZO YA TATHMINI YA ATHARI KWA MAZINGIRA

 

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia kurugenzi ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii imetoa mafunzo ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira kwa wataalamu elekezi wa mazingira na watumishi wa Baraza waliopo Kanda ya Magharibi inayohusisha mikoa mitatu (Kigoma, Katavi na Tabora) kuanzia tarehe 1-3 Oktoba, 2025.

Mafunzo haya ni endelevu na lengo kuu ni kuboresha ufanyaji wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) na upitiaji wa taarifa za TAM zinazowasilishwa Baraza.

NEMC, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA NISHATI NA PURA WATEMBELEA MAMLAKA YA MAZINGIRA NCHINI NORWAY KUJADILI NISHATI KWA MAENDELEO ENDELEVU

Pichani ni ujumbe wa Tanzania ukiwajumuisha maafisa kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Wizara ya Nishati na PURA uliotembelea ofisi za Mamlaka ya Mazingira ya Norway (Norwegian Environment Agency-NEA) kubadilishana uzoefu na kujadili fursa za ushirikiano chini ya mpango wa Nishati kwa Maendeleo (Energy for Development).

Ziara hii imelenga kuimarisha ushirikiano katika udhibiti wa uchafuzi, taarifa za mabadiliko ya tabianchi na maendeleo yenye uzalishaji mdogo wa hewa chafuzi.

Kupitia mpango wa Nishati kwa Maendeleo (Energy for Development - EfD), NEA inashirikiana na nchi za Afrika zikiwemo Tanzania, Nigeria, Msumbiji, Malawi, Uganda, Ghana na Afrika Kusini. Ushirikiano wa sasa kati ya Tanzania na Norway unalenga udhibiti wa uchafuzi wa mazingira na utoaji wa taarifa za hali ya hewa, lakini unaweza kuongezwa baada ya mwaka 2026 kujumuisha maeneo mapana zaidi kama mabadiliko ya tabianchi, bayoanuai na usimamizi wa uchafuzi

Mamlaka ya Mazingira ya Norway (Norwegian Environment Agency - NEA) ndiyo taasisi kuu inayotekeleza sera za mazingira za Norway chini ya Wizara ya Hali ya Hewa na Mazingira. Muundo wake wa uongozi ni rahisi, Serikali, Wizara, NEA, Magavana na Halmashauri za Manispaa na inatoa ushauri kuhusu mabadiliko ya tabianchi, bayoanuai, uchafuzi wa mazingira na matumizi ya ardhi. NEA pia huandaa Ripoti za Hali ya Mazingira, hutoa kanuni na vibali, na kushirikiana kitaifa na kimataifa.

Mfumo wa kisheria wa Norway wa udhibiti wa hewa chafu unajumuisha Sheria ya Udhibiti wa Uchafuzi (Pollution Control Act, 1993), Usalama na Mazingira (HSE) kwa shughuli za mafuta na gesi, Kanuni za Uchafuzi na Taka, Vibali vya Udhibiti wa Uchafuzi, Sheria ya Biashara ya Uzalishaji wa Gesi Joto (Greenhouse Gas Emissions Trading Act), na Sheria ya Ulinzi wa Uanuai (Nature Diversity Act). Sheria hizi huipa NEA mamlaka ya kudhibiti utoaji wa gesi chafuzi kama methane na kabonidaioksaidi (CO2) na kuhakikisha ufuatiliaji na utekelezaji wa masharti kwa sekta mbalimbali, zikiwemo mafuta na taka.

Kwa kadirio la uzalishaji wa methane kutoka dampo na maeneo ya utupaji taka, NEA hutumia mbinu za Shirika la Kiserika

 Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) leo tarehe 26, Septemba, 2025 limefanya Kikao na wadau kutoka Benki ya Dunia ili kujadili fursa za mazingira zinazoweza kuchangia katika uongezaji wa thamani kwenye shughuli za utafiti, uchimbaji na uchenjuaji wa madini.

Majadiliano hayo yaliyoongozwa na Meneja wa NEMC-Kanda ya Ziwa Magharibi Bw. Boniface Guni ambayo yalilenga kutambua kwa ujumla majukumu ya NEMC na vipaumbele vyake katika sekta ya Madini.

Meneja wa NEMC-Kanda ya Ziwa Magharibi Bw. Boniface Guni (kulia) akizungumza katika Kikao hicho

Wataalamu kutoka Benki ya Dunia wakiwa katika Kikao hicho kilichofanyika tarehe 26, Septemba, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa NEMC Jijini Dar es Salaam

NEMC YAADHIMISHA SIKU YA AFYA MAZINGIRA DUNIANI, ELIMU YA MAZINGIRA YATOLEWA SHULENI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika kuadhimisha Siku ya Afya mazingira Duniani, Leo tarehe 26 Septemba limetembelea  Shule ya Msingi Mikocheni "A" na kutoa elimu ya Afya na Mazingira kwa wanafunzi na walimu ambapo kaulimbiu kwa mwaka huu 2025 ni "Tokomeza taka za plastiki, Jenga jamii yenye afya Bora.

Elimu hiyo imejikita katika kuhamasisha utunzaji wa mazingira shuleni, pamoja na kuelezea Dhana ya Punguza, Tumia tena na Rejeleza katika Udhibiti wa taka ikiwa ni pamoja na kufundisha kuhusu usafi wa mwili na mazingira ya nyumbani. 

Afisa Mazingira wa NEMC Bi. Rukia Ally akitoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Mikocheni "A" katika Maadhimisho ya Siku ya Afya Mazingira Duniani tarehe 26, Septemba.

Wanafunzi walishirikiana kwa kuuliza maswali na kujifunza mbinu rahisi za kuhakikisha mazingira yao yanabaki safi na salama kwa wote.

Aidha, maafisa hao walitoa wito kwa jamii nzima kushirikiana katika kuendeleza jitihada za kulinda mazingira, kwani afya njema haiwezi kupatikana endapo mazingira yanaharibika. Waliwataka wazazi, walimu na viongozi wa jamii kuhakikisha elimu hiyo inapelekwa hadi majumbani na maeneo ya kazi, ili kila mmoja awe balozi wa mazingira bora.

Hivyo basi, maadhimisho ya Siku hii yamekuwa chachu ya kuimarisha mshikamano wa pamoja katika kuyalinda mazingira kwa mustakabali endelevu wa kizazi cha sasa na kijacho.

Maafisa wa NEMC wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Mikocheni A mara baada ya kutoa elimu ya Mazingira kwa wanafunzi wa Shule hiyo ikiwa ni sehemu ya Kuadhimisha Siku ya Afya Mazingira Duniani

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mikocheni A wakifuatilia Elimu iliyotolewa na Maafisa Mazingira kutoka NEMC katika Maadhimisho ya Siku ya Afya Mazingira Duniani

NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...