Nyumbani

๐๐„๐Œ๐‚ ๐˜๐€๐„๐๐ƒ๐„๐’๐‡๐€ ๐Œ๐€๐…๐”๐๐™๐Ž ๐Š๐”๐‡๐”๐’๐” ๐๐˜๐„๐๐™๐Ž ๐™๐€ ๐”๐’๐ˆ๐Œ๐€๐Œ๐ˆ๐™๐ˆ ๐–๐€ ๐Œ๐€๐™๐ˆ๐๐†๐ˆ๐‘๐€ ๐Š๐–๐€ ๐–๐ˆ๐™๐€๐‘๐€, ๐“๐€๐€๐’๐ˆ๐’๐ˆ ๐๐€ ๐‡๐€๐‹๐Œ๐€๐’๐‡๐€๐”๐‘๐ˆ ๐™๐€ ๐Œ๐€๐๐ˆ๐’๐๐€๐€ ๐๐€ ๐–๐ˆ๐‹๐€๐˜๐€

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linaendeaha mafunzo kuhusu nyenzo za usimamizi wa mazingira kwa Wizara, Taasisi pamoja na Halmashauri za Manispaa na Wilaya nchini. Mafunzo haya yameandaliwa kupitia Mradi wa kujenga uwezo wa kitaifa katika kusimamia Sheria ya usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004. Mradi huu unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA). Mradi unalenga kuimarisha uelewa na uwezo wa watumishi katika kusimamia Sheria ya mazingira kwa ufanisi katika utekelezaji wa majukumu katika maeneo yao ya kazi.


Mafunzo hayo ya siku mbili yameanza tarehe 27 na kumalizika 28 Novemba 2025 jijini Dodoma. Kupitia mafunzo haya, washiriki wanapata maarifa ya kutathmini athari za kimazingira pamoja na kupanga mikakati endelevu ya utunzaji wa mazingira huku wakizingatia Nguzo ya tatu ya Dira ya maendeleo ya Taifa 2050 ambayo imeweka mkazo juu ya kuzingatia masuala ya utunzaji wa Mazingira nchini.

Akifungua mafunzo hayo, Meneja wa maeneo maalum na mabadiliko ya tabianchi kutoka NEMC, Dkt. Careen Kahangwa, aliwataka washiriki kutumia fursa hiyo kuboresha utendaji katika maeneo yao ya kazi. Mafunzo haya yanaendeshwa na timu ya wataalamu kutoka NEMC. Aidha wataalamu kutoka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ofisi ya Makamu wa Rais na taasisi binafsi ya Taka ni ajira nao walishiriki Katika kutoa mafunzo.

Washiriki wa mafunzo hayo wamepata nafasi ya kujadili kwa kina changamoto za kimazingira zinazojitokeza katika taasisi zao na kujifunza mbinu bora za kukabiliana nazo. Kupitia mafunzo haya, wanatarajiwa kuboresha mifumo ya ufuatiliaji, utoaji taarifa, na utekelezaji wa sheria na kanuni za mazingira nchini. Hatua hii muhimu itachangia kwa kiasi kikubwa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.







๐ƒ๐Š๐“. ๐…๐„๐’๐“๐Ž ๐ƒ๐”๐†๐€๐๐†๐„ ๐€๐™๐”๐๐†๐”๐Œ๐™๐€ ๐๐€ ๐–๐€๐“๐”๐Œ๐ˆ๐’๐‡๐ˆ ๐–๐€ ๐๐„๐Œ๐‚

๐€๐ฌ๐ข๐ฌ๐ข๐ญ๐ข๐ณ๐š ๐”๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข ๐ง๐š ๐”๐ฌ๐ข๐ฆ๐š๐ฆ๐ข๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐Œ๐š๐ณ๐ข๐ง๐ ๐ข๐ซ๐š ๐ก๐š๐ฌ๐š ๐ฎ๐๐ก๐ข๐›๐ข๐ญ๐ข ๐ฐ๐š ๐ค๐ž๐ฅ๐ž๐ฅ๐ž ๐œ๐ก๐š๐Ÿ๐ฎ๐ณ๐ข ๐ฆ๐š๐ž๐ง๐ž๐จ ๐ฒ๐š ๐ฆ๐š๐ค๐š๐ณ๐ข


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais  (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Festo Dugange, amefanya ziara yake ya kwanza katika Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na kuzungumza na watumishi wa Baraza hilo, akitoa maelekezo mahsusi juu ya kuimarisha usimamizi wa mazingira nchini.

Katika hotuba yake, Dkt. Dugange amesisitiza umuhimu wa kulinda afya ya jamii kupitia udhibiti wa kelele chafuzi, akibainisha kuwa kelele zimekuwa chanzo cha changamoto za kiafya, hususani magonjwa yasiyoambukiza katika maeneo ya makazi.

Amesema kelele chafuzi ni miongoni mwa mambo yanayoashiria uharibifu wa mazingira na yanapaswa kudhibitiwa kwa nguvu na umakini wa hali ya juu.

Akiweka msisitizo zaidi, Dkt. Dugange ameagiza NEMC kuandaa mpango mkakati wa mashirikiano  kati yake na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) hasa kwenye majiji  ili kuhakikisha udhibiti wa kelele chafuzi unatekelezwa katika ngazi zote kutoka Mtaa hadi Taifa. 

Amesisitiza  kuwa kila mtumishi wa NEMC ana jukumu la kuhakikisha jamii inajengewa uelewa na Sheria za Mazingira zinatekelezwa ipasavyo.

Katika mazungumzo hayo, Dkt. Dugange pia ameuzungumzia Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2050 unaohusisha nguzo tatu kuu, ikiwemo Uhifadhi wa Mazingira na Ustahimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi

Amefafanua uhusiano uliopo kati ya mazingira salama, afya bora, na kupungua kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Akigusia ajenda ya nishati safi, Dkt. Dugange alikumbusha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inataka ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ambayo ina manufaa kwa jamii ikiwemo kupunguza uchafuzi wa hewa, kulinda mazingira na kupunguza gharama za maisha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Mhandisi Mwanasha Tumbo, ameahidi kusimamia utekelezaji wa maelekezo yote yaliyotolewa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt.Immaculate Sware Semesi amepokea maelekezo na kuahidi kuyatekeleza kwa mujibu wa Sheria na kuhakikisha usimamizi thabiti wa mazingira nchini.



๐๐„๐Œ๐‚ ๐˜๐€๐ˆ๐‹๐€๐™๐€ ๐–๐‚๐… ๐Ÿ“ ๐๐ˆ๐‹๐€ ๐’๐‡๐ˆ๐Œ๐Œ๐”๐“๐€ ๐Ÿ๐ŸŽ๐Ÿ๐Ÿ“

Timu ya mpira wa miguu ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) imeilaza timu ya WCF kwa jumla ya magoli matano kwa sifuri.

Mchezo huo uliochezwa Novemba 27, 2025, katika uwanja wa Highland mkoani Morogoro, ulianza kwa kasi kubwa ambapo dakika ya 15 Fortinatus Patrick alifungua ukurasa wa mabao kupitia mkwaju wa penati, na kufanya “mazingira ya uwanja” kuanza kuwa safi. Bao hilo lilidumu hadi dakika ya 33 ambapo mfungaji huyo huyo, Fortinatus Patrick, alipachika bao la pili lililoipeleka NEMC mapumzikoni wakiwa kifua mbele, huku “mazingira” yakiendelea kupendeza uwanjani.

Kipindi cha pili kilipoanza dakika ya 46, Fortinatus Patrick aliendeleza ubabe kwa kufunga bao la tatu, kabla ya kiungo Ismail Jemba kuongeza la nne dakika ya 51.

Kama ilivyo desturi ya NEMC kutoridhishwa na uchafuzi wa mazingira nchini na kuendelea kuhimiza usafi kote nchini, vivyo hivyo hawakuridhika na matokeo hayo ya 4–0. Dakika ya 62, Emmanuel Mlungwana alipiga shuti kali kutoka katikati ya uwanja lililopenya kati ya miguu ya golikipa wa WCF na kutinga wavuni, likiwa bao la tano kwa NEMC.

NEMC ipo mkoani Morogoro kushiriki michezo ya SHIMMUTA 2025 kama sehemu ya kuimarisha afya za watumishi wake pamoja na kuendelea kutoa hamasa kuhusu uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini. Kwa mwaka huu, timu za NEMC zimefadhiliwa jezi na vifaa vya michezo kupitia miradi yake miwili — Adaptation Fund na EHPMP — huku zikitumia jezi hizo kueneza jumbe mbalimbali kuhusu mabadiliko ya tabianchi na udhibiti wa matumizi ya zebaki (mercury).




NEMC YAELIMISHA UMMA UDHIBITI WA KELELE CHAFUZI NA MITETEMO

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeendelea kuimarisha juhudi za kudhibiti uchafuzi wa mazingira unaotokana na kelele na mitetemo kufuatia ongezeko la malalamiko katika maeneo ya mijini na vijijini. 

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Bw. Hamadi Taimuru, Meneja wa Uzingatiaji wa Sheria (NEMC), amesema kelele zimeendelea kuwa changamoto kubwa kwa afya na ustawi wa wananchi kutokana na shughuli za burudani, ujenzi, biashara na matumizi ya vifaa vya sauti vinavyokiuka viwango vya kisheria.


Meneja wa Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bw. Hamadi Taimuru akizungumza na vyombo vya habari alipokuwa akitoa taarifa kwa umma kuhusu kelele chafuzi na mitetemo

Bw. Taimuru amefafanua kuwa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (Sura 191) na Kanuni za Udhibiti wa Kelele na Mitetemo za mwaka 2015 zimeweka viwango maalumu vya kelele kwa maeneo ya makazi, biashara, viwanda na Taasisi muhimu kama Hospitali na shule, sambamba na kuainisha utaratibu wa utoaji vibali kwa shughuli zinazoweza kusababisha kelele kubwa. 

Amesema athari za kelele za muda mrefu ni pamoja na kupoteza usikivu, msongo wa mawazo, shinikizo la damu na kuathiri umakini wa watoto shuleni, hivyo kulifanya suala la udhibiti kuwa muhimu kwa kulinda afya ya umma".

Aidha, amebainisha uwepo wa changamoto mbalimbali katika utekelezaji wa Kanuni za udhibiti, ikiwemo uhaba wa vifaa vya kupimia kelele kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, uelewa mdogo wa wananchi kuhusu athari za kelele, pamoja na baadhi ya biashara na maeneo ya burudani kutokufuata sheria na muda wa utulivu. 

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, viwango vinavyoruhusiwa ni 70dBA mchana na 60dBA usiku kwa maeneo ya viwandani; 50dBA mchana na 35dBA usiku kwa makazi, 60dBA mchana na 50dBA usiku kwa makazi yenye viwanda vidogo,  55dBA mchana na 45dBA usiku kwa maeneo ya makazi, biashara na burudani; na 45dBA mchana na 35dBA usiku kwa Hospitali, Shule, Kumbi za mikutano na maeneo ya mapumziko.

Katika kuimarisha usimamizi, Bw. Taimuru alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya OSHA, Polisi, BASATA, Serikali za Mitaa, nyumba za ibada na wamiliki wa kumbi za burudani katika kutekeleza majukumu yao, ikiwemo kusimamia vibali, kutoa elimu, kuhakikisha matumizi sahihi ya vifaa vya sauti na kufanya kaguzi za mara kwa mara.

Aliongeza kuwa ramani za viwango vya kelele, kampeni za uelimishaji na mifumo rahisi ya utoaji taarifa za malalamiko ni hatua muhimu zinazohitajika kuimarishwa.

Akihitimisha, Bw. Hamadi Taimuru amesema Tanzania ina mfumo madhubuti wa kisheria wa kudhibiti kelele na mitetemo, na kwamba ushirikiano wa wadau wote, sekta binafsi, Taasisi za umma na wananchi ni msingi muhimu wa kulinda afya, utulivu na ustawi wa jamii.

๐๐„๐Œ๐‚ ๐˜๐€๐„๐๐ƒ๐„๐’๐‡๐€ ๐Œ๐€๐…๐”๐๐™๐Ž ๐˜๐€ ๐๐ƒ๐€๐๐ˆ ๐‰๐”๐” ๐˜๐€ ๐Œ๐€๐๐ˆ๐“๐ˆ๐Ž ๐˜๐€ ๐“๐€๐€๐‘๐ˆ๐…๐€ ๐™๐€ ๐“๐€๐“๐‡๐Œ๐ˆ๐๐ˆ ๐˜๐€ ๐€๐“๐‡๐€๐‘๐ˆ ๐Š๐–๐€ ๐Œ๐€๐™๐ˆ๐๐†๐ˆ๐‘๐€ ๐๐€ ๐‰๐€๐Œ๐ˆ๐ˆ ๐๐€ ๐Š๐€๐†๐”๐™๐ˆ ๐™๐€ ๐Œ๐€๐™๐ˆ๐๐†๐ˆ๐‘๐€

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Kurugenzi ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii limeendelea kujenga uwezo kwa watumishi wake kwa kuendesha mafunzo ya ndani yahusuyo mapitio ya taarifa za Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) pamoja na kaguzi za mazingira. 

Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika kuanzia tarehe 18 hadi 21 Novemba 2025 yakilenga kuongeza weledi na kuimarisha utendaji katika kupitia taarifa na kufanya kaguzi za miradi inayowasilishwa kwa Baraza, kuimarisha umahiri wa watumishi hao na kuandaa timu madhubuti yenye uwezo wa kushughulikia kwa haraka na kwa ubora wa juu taarifa za tathmini na kaguzi za mazingira zinazowasilishwa na wawekezaji kwa Baraza.

Mkurugenzi wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (NEMC) Bi. Lilian Lukambuzi akiwasilisha mada katika mafunzo hayo
Mafunzo haya yalifunguliwa rasmi na Mkurugenzi wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii, Bi. Lilian Lukambuzi, na kuendeshwa na wataalamu kutoka ndani ya Kurugenzi hiyo wakiwemo Eng. Luhuvilo Mwamila "Kaimu Meneja Mapitio ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii" na Bi. Edika Masisi "Meneja Usajili wa Wataalamu Elekezi wa Mazingira". Washiriki walipata nafasi ya kujifunza kwa undani namna bora za kufanya mapitio ya taarifa za TAM, vigezo vya tathmini, na hatua muhimu katika ukaguzi wa mazingira ili kuhakikisha miradi inazingatia sheria ya Mazingira.

Aidha, mafunzo hayo yaliwalenga watumishi wa NEMC kutoka kanda za Mashariki Kaskazini, Mashariki Kusini, Ilala, Temeke, Bagamoyo pamoja na Makao Makuu.














NEMC YASHIRIKI UNFCCC COP- 30, BELEM, NCHINI BRAZIL, USHIRIKI WAKE KULETA MANUFAA KWENYE MIRADI NA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki Mkutano wa thelathini wa nchi wanachama wa Mkataba wa Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (UNFCCC COP-30), unaoendelea jijini Bรฉlem, nchini Brazil kuanzia tarehe 03/11/2025 na unatarajiwa kukamilika tarehe 21/11/2025.
Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC Mhandisi Mwanasha Tumbo (wa pili kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na timu ya NEMC iliyoshiriki Mkutano huo na baadhi ya washiriki kutoka mataifa mengine. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi

Akiongoza ujumbe wa NEMC katika Mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Mhandisi Mwanasha Tumbo aliyeambatana pia na Makamu Mwenyekiti, Wakili Alex G. Mgongolwa aliwataka watumishi wa Baraza kuhakikisha wanatumia vyema jukwaa la mkutano huo kupata fursa za fedha za miradi ili kuweza kuhakikisha unaleta matokeo chanya katika kutekeleza vyema nguzo ya mazingira katika Dira ya Taifa ya 2050.

Katika kutekeleza hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi, ameongoza ujumbe wa NEMC kwenye Mikutano mbalimbali ya uwili ili kuimarisha ushirikiano na wadau katika sekta ya Mazingira. 

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akizungumza katika Mkutano huo
Baadhi ya Mikutano hiyo ni pamoja na mkutano wa uwili na Benki ya Maendeleo ya Africa (African Development Bank), uliohusu kuanza kwa mradi uliowasilishwa na Baraza na kupitishwa na benki hiyo. Mradi huo wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 15 unatarajiwa kutatua changamoto za mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya pwani yaani Dar es Salaam, Pwani na Pemba. 

Aidha, Dkt. Semesi alikutana pia na Sekretarieti ya Mfuko wa Kimataifa wa kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi (Adaptation Fund-AF) ambapo aliweza kuwahimiza Adaptation Fund kukamilisha taratibu za kulipatia Baraza ithibati ya pili (reaccreditation) sambamba na kukamilisha mapitio ya miradi iliyowasilishwa yenye jumla ya thamani ya Dola za Marekani milioni 35. Katika mazungumzo hayo, mfuko wa  Adaptation Fund umelihakikishia Baraza kwamba taratibu za ithibati zitakamilika ndani ya wiki chache kuelekea mwishoni mwa mwaka huu. 

Hata hivyo Adaptation Fund umeidhinisha ripoti za mwaka za miradi ya SWAHAT na Bunda inayosimamiwa na Baraza Pamoja na kuachilia kiasi cha takribani Dola za Marekani laki 4 ili kukamilisha utekelezaji wa miradi hiyo.

Mtaalam wa Mazingira (NEMC) ndugu. Paul Kalokola akifafanua jambo katika Mkutano huo
Sambamba na hayo, Dkt. Semesi ameongoza ushiriki katika vikao mbalimbali vya kitaalam, mikutano ya pembezoni pamoja na kuanzisha mchakato wa mashirikiano na taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi ili kupanua wigo wa kujipatia fedha za kupambana na mabadiliko ya tabianchi. Baadhi ya taasisi hizo ni pamoja na Mfuko wa Kitaifa wa Maji (National Water Fund), Pew Charitable Trust, Benki ya Dunia, Global Climate Mobility, Global Methen Hub, IUCN na Ocean Vision.

Timu ya wataalam iliyoambatana na ujumbe wa Bodi kwenye Mkutano huo ni pamoja na Dkt Careen Kahangwa, Bw. Fredrick Mulinda, Bw, Paul Kalokola, Bi. Jackline Nyantori na Bw. Rahim Kantinga.

NEMC YASHIRIKI KIKAO KAZI CHA KUPITIA MPANGO WA KITAIFA WA KUPAMBANA NA UKAME

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikao kazi cha kupitia Mpango wa Kitaifa wa kupambana na ukame kilichofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), mkoani Morogoro.
Akizungumza katika kikao hicho, muwakilishi kutoka NEMC ambaye pia ni Afisa Mazingira Mkuu Bi.Marlene Moshi amesema ushiriki wa NEMC ni muhimu katika kuhakikisha kuwa mikakati ya kitaifa inakwenda sambamba na malengo ya kimataifa ya kupunguza athari za ukame na kulinda mazingira.

Kikao hicho kimeratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais (VPO) kupitia Idara ya Mazingira, kikilenga kuhakikisha utekelezaji wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kupambana na Kuenea kwa Jangwa na Ukame Duniani.


NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...