Elimu ya Mazingira ikitolewa katika banda la NEMC katika Kongamano la Vijana lililofanyika katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Juni 2, 2026 lenye kauli mbiu "Ushiriki wa Vijana katika Kutekeleza Dira 2050: Usimamizi Endelevu wa Mazingira na Uhimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi"
WAZIRI MASAUNI AZURU BANDA LA NEMC KONGAMANO LA VIJANA LILILOFANYIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
Elimu ya Mazingira ikitolewa katika banda la NEMC katika Kongamano la Vijana lililofanyika katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Juni 2, 2026 lenye kauli mbiu "Ushiriki wa Vijana katika Kutekeleza Dira 2050: Usimamizi Endelevu wa Mazingira na Uhimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi"
NEMC YASHIRIKI KONGAMANO LA VIJANA KUJADILI USIMAMIZI ENDELEVU WA MAZINGIRA NA DIRA 2050
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeungana na wadau mbalimbali wa Mazingira kushiriki Kongamano la Vijana lililofanyika Juni 2, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), likiwa na kaulimbiu isemayo "Ushiriki wa Vijana katika Kutekeleza Dira 2050: Usimamizi Endelevu wa Mazingira na Uhimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi."
Akifungua kongamano hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yusuf Masauni, amesisitiza umuhimu wa vijana kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi ili kuhakikisha maendeleo endelevu na utekelezaji wenye mafanikio wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Kupitia kongamano hilo, NEMC imepata fursa ya kutoa elimu ya mazingira kwa vijana, kuhamasisha matumizi endelevu ya rasilimali na kujadili nafasi ya vijana katika kuibua suluhisho bunifu za kukabiliana na changamoto za mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa maendeleo ya Taifa ya sasa na vizazi vijavyo.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MHE. REUBEN KWAGILWA AZURU BANDA LA NEMC MAONESHO KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Reuben Kwagilwa (wa katikati kulia) azuru Banda la NEMC Maadhimisho ya wiki ya Mazingira Duniani, katika viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Center (JKCC) Jijini Dodoma ambapo leo tarehe 1 Juni ndio ufunguzi wa maonesho hayo. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Baraka Luvanda.
MWENYEKITI WA BODI YA NEMC AZUNGUMZA NA WADAU WA MAZINGIRA, NEMC@40
Mwenyekiti wa Bodi ya NEMC, Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka Arobaini (40) ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) yaliyofanyika tarehe 29 Mei 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo hayo, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa wadau mbalimbali katika kulinda na kuhifadhi mazingira, akieleza kuwa mafanikio ya NEMC katika kipindi cha miaka 40 yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na ushiriki wa serikali, sekta binafsi, taasisi na wananchi.
Aidha, ametoa wito wa kuendelea kuwekeza katika elimu ya mazingira, matumizi ya teknolojia na utekelezaji wa sheria ili kuhakikisha mazingira yanalindwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.
𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗬𝗔𝗞𝗨𝗧𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔 𝗪𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗔𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔 𝗚𝗥𝗘𝗘𝗡 𝗦𝗨𝗠𝗠𝗜𝗧 𝟮𝟬𝟮𝟲
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekutana na ujumbe wa waandaaji wa Tanzania Green Summit (TGS), inayotarajiwa ...
-
Ni katika kufanya tathmini na kuimarisha umoja. Watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Makao Makuu na k...
-
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Kusini tarehe 15 Novemba 2025 lilishiriki kusimamia na kushuhudia Uteke...
-
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...