Nyumbani

NEMC KANDA YA KUSINI YATOA ELIMU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA - MTWARA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Kanda ya Kusini limetoa elimu ya uhifadhi wa mazingira kwa jamii ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, tarehe 15 Agosti 2026, kuhusu umuhimu wa kulinda mazingira, wajibu wa jamii katika uhifadhi wa mazingira na fursa za kiuchumi zinazotokana na usimamizi endelevu wa mazingira katika Mkoa wa Mtwara na mikoa jirani.

Elimu hiyo imetolewa kwa wananchi kupitia Dira Mpya Group na Star Women, vikundi vinavyojishughulisha na usafi wa mazingira na ujasiriamali. Mafunzo hayo yameongozwa na Meneja Ngowo Gift, akishirikiana na Dkt. Kharid Mwakoba na Obasanjo Nniwako kutoka NEMC.


Katika mafunzo hayo, wananchi wameelimishwa kuhusu umuhimu wa kulinda mazingira na kuchukua hatua za kuzuia uharibifu wa mazingira, sambamba na kutambua fursa mbalimbali za kiuchumi zinazotokana na matumizi na usimamizi endelevu wa rasilimali za mazingira.

Katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Uhifadhi wa Mazingira na Ustahimilivu dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi ni Nguzo ya Tatu ya Dira hiyo. Hivyo, mazingira si suala la pembeni katika maendeleo ya Taifa, bali ni sehemu ya msingi ya Tanzania tunayoijenga kwa maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi.

Juhudi za utoaji wa elimu ya mazingira zinazoendelea kufanywa na NEMC zinalenga kujenga jamii yenye uelewa na uwezo wa kutambua athari za uharibifu wa mazingira, kuchukua hatua za kuzuia na kudhibiti madhara, pamoja na kutumia fursa zinazotokana na usimamizi endelevu wa mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

NEMC inaendelea kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa mazingira, kwa kutambua kuwa mazingira salama ni msingi wa afya, maendeleo na uchumi endelevu wa Taifa







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC KANDA YA KUSINI YATOA ELIMU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA - MTWARA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupitia Kanda ya Kusini limetoa elimu ya uhifadhi wa mazingira kwa jamii ya Mani...