Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeongeza vyombo vya usafiri kwa kutumia mapato yake ya ndani, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha miundombinu wezeshi ya utekelezaji wa majukumu ya kimazingira, ikiwemo ufuatiliaji, ukaguzi na uzingatiaji wa Sheria ya mazingira nchini.
Akizungumza leo Agosti 11, 2026 wakati wa makabidhiano ya magari mawili kwa baadhi ya viongozi wa Baraza, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, amesema Baraza limeanza na magari mawili kati ya matano kwa ajili ya viongozi na linatarajia kununua magari mengine 20 ndani ya mwaka huu kwa ajili ya kuimarisha utendaji kazi katika Kanda zote 13 nchini.
“Magari haya tumeyanunua sisi wenyewe kwa kutumia mapato yetu ya ndani na tunaanza na magari 5 kwa ajili ya viongozi, lakini kwa malengo tuliyojiwekea kwa mwaka huu tutanunua magari mengine 20 " amesema Dkt. Semesi.
Ameongeza “Hii ni katika kuhakikisha tunaboresha utendaji kazi katika jukumu tulilokasimiwa la usimamizi wa mazingira nchini, sawa na malengo na matakwa ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 pamoja na malengo ya Rais wetu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan,”
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Fedha Bw. Dickson Mjinja alipozungumza aliahidi utunzwaji wa magari hayo na kutumika kwa malengo kusidiwa huku akisistiza uwajibikaji kufikia
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni