Nyumbani

𝗠𝗪𝗘𝗡𝗬𝗘𝗞𝗜𝗧𝗜 𝗪𝗔 𝗕𝗢𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗔𝗞𝗜𝗠𝗕𝗜𝗔 𝗞𝗜𝗟𝗢𝗠𝗜𝗧𝗔 𝟱

Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mhandisi Mwanasha Tumbo, ameshiriki mbio za kilomita 5 zilizofanyika katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani. 


Mbio hizo zililenga kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira na kuendeleza afya kupitia shughuli za michezo.

Tukio hilo liliwakutanisha viongozi wa Serikali, wadau wa mazingira na wananchi mbalimbali, likibeba ujumbe wa pamoja wa kulinda mazingira kwa maendeleo endelevu na ustawi wa vizazi vya sasa na vijavyo.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NEMC YASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI-DODOMA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kikamilifu kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliy...