📌Yamshukuru Dkt. Semesi kwa kuwaamini na kuwateua kuratibu Maadhimisho hayo
Kamati ya Maadhimisho ya Miaka 40 ya NEMC ambayo ilihusika katika maandalizi ya sherehe hiyo ambayo kilele chake kilikuwa Mei 28 na 29, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), imekabidhi taarifa ya Maadhimisho hayo kwa Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi leo Agosti 19,2026.
Akizungumza wakati wa kukabidhi taarifa hiyo ya Maadhimisho, Mwenyekiti wa Kamati ya NEMC@40 Bi. Juliana Masawe ambaye pia ni Afisa Utumishi Mkuu wa NEMC amemshukuru Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi kwa kuiamini Kamati hiyo na kuipa jukumu hilo kubwa la kihistoria nchini.
Bi. Juliana amesisitiza kuwa kila kilichofanywa na Kamati hiyo ni kupitia maono ya Dkt. Semesi yaliyowarahisishia kutekeleza jukumu hilo kwa ufanisi na weledi na kufanya Maadhimisho hayo kufanikiwa kwa viwango vya juu.
Akipokea taarifa hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi ameishukuru Kamati hiyo kwa kutomuangusha katika kutekeleza jukumu hilo na amewataka kuendelea kuwa mfano bora kwa wengine katika kutekeleza majukumu wanayopangiwa.
Kamati ya NEMC@40 ilikuwa ikiongozwa na Mwenyekiti Juliana Masawe, Katibu Paul Kalokola, Wajumbe ni Tajiri Kihemba, Albert Mgoye, Roselyne Mayowa, Rahim Kantinga, Upendo Mtunguja, Cecilia Douglas, Fredrick Mulinda, Shukrani Haule, Elibariki Bajuta na Mosses Nonga.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni