Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ni miongoni mwa taasisi zinazoshiriki katika Warsha ya Wadau inayofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 17 hadi 20 Agosti 2026. Warsha hiyo imeandaliwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupitia Mradi wa Barabara kwa Ujumuishaji na Fursa za Kijamii na Kiuchumi (RISE).
Warsha hiyo inalenga kufanya mapitio na uboreshaji wa Rasimu ya Mpango wa Kitaifa wa Utekelezaji wa Uhimilivu dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi (NCCR-AP) pamoja na Miongozo ya Utekelezaji kwa Sekta ya Barabara nchini Tanzania.
Lengo kuu la warsha ni kukusanya maoni na michango kutoka kwa wadau mbalimbali ili kuboresha nyaraka hizo na kuhakikisha zinatoa mwongozo madhubuti wa kuimarisha uhimilivu wa miundombinu ya barabara dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi nchini Tanzania.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni