Nyumbani

NEMC YASHIRIKI WARSHA YA KUJADILI UREJESHWAJI IKOLOJIA YA MATUMBAWE

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki Warsha ya kujadili namna bora ya urejeshwaji wa mifumo ikolojia ya matumbawe iliyofanyika Zanzibar kuanzia tarehe 16-17 Septemba 2025. 

NEMC imewakilishwa na Meneja wa Tafiti za Mazingira (NEMC), Dkt. Rose Sallema Mtui, ambaye pia ni Mratibu wa Kikosi kazi cha Taifa cha kuhifadhi na kutunza matumbawe. 

Kikao hicho kimeratibiwa na shirika la Uhifadhi Mazingira la “The Nature Conservancy”

Meneja wa Tafiti za Mazingira (NEMC) Dkt. Rose Sallema akiwasilisha mada katika Warsha hiyo

Baadhi ya washiriki wa Warsha hiyo wakifuatilia mada zilizowasilishwa katika Warsha hiyo




Baadhi ya wawasilishaji wakiwasilisha mada katika Warsha hiyo


Washiriki wa Warsha ya kujadili namna bora ya urejeshwaji wa mifumo ikolojia ya matumbawe wakiwa katika picha ya pamoja, Warsha hiyo imefanyika Zanzibar kuanzia tarehe 16-17 Septemba 2025. 

NEMC YASHIRIKI WASILISHO LA RIPOTI YA MAKUNDI MAALUM KUTOKA KWA ASASI YA WATED JIJINI DODOMA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), limeshiriki uwasilishaji wa ripoti ya mchango wa wanawake, wasichana na makundi yaliyo pembezoni kwenye sera ya Taifa ya Ardhi 1995 (Toleo la 2023) na mchakato wa NDC 3.0V  uliofanyika katika ukumbi wa Residence Jijini Dodoma leo.

Akiwasilisha ripoti hiyo iliyoandaliwa kwa kushirikiana na WAHEAL na  Tree of Hope, Mkurugenzi wa Asasi ya Kiraia kutoka Women Action Towards Entrepreneurship Development (WATED) Bi. Maria Matui amesema imelenga kuainisha changamoto za wanawake wa vijijini pamoja na kusaidia jitihada za mashirika katika kupaza sauti za wanawake kwenye masuala ya usimamizi wa ardhi na harakati za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Walioshiriki katika uwasilishaji wa ripoti Asasi ya WATED ya mchango wa wanawake, wasichana na makundi wakiwa katika picha ya pamoja .

 
Amesema wasilisho hilo lililohusisha pia wanachama wa mtandao wa mabadiliko ya tabianchi limeainisha changamoto nyingi wanazopitia wanawake wa vijijini zikiwemo, mila na desturi, mitazamo na mifumo dume hali inayoathiri masuala ya maendeleo hasa shughuli za uzalishaji.
Baadhi ya washiriki wa wasilisho la Asasi ya WATED wakiwa 
 katika ukumbi wa Residence leo Septemba 17, 2025  Dodoma 

Malengo makubwa matatu yaliyowasilishwa ni pamoja na kuweka wazi mchango wa wanawake, wasichana na makundi yaliyo pembezoni katika utekelezaji wa Sera ya Ardhi ya 1995(Toleo la 2023, kushirikiana na Serikali katika kuboresha mchakato wa NDC.3.0V kwa kuzingatia usawa wa kijinsia na haki za makundi yote ya jamii pamoja na kutoa mapendekezo Sera shirikishi yatakayohakikisha usimamizi endelevi wa rasilimali na upatikanaji wa haki sawa kwa kila mmoja.

Baadhi ya washiriki wa wasilisho la Asasi ya WATED wakifuatilia wasilisho hilo lililofanyika  katika ukumbi wa Residence leo Septemba 17, 2025  Dodoma 

Mikoa iliyofikiwa na Asas hizi ni pamoja na Ruvuma, Morogoro, Kilimanjaro, Geita, Arusha, Mara, Kagera na Tanga.

NEMC NA TAASISI MBALIMBALI WAADHIMISHA SIKU YA MIKOKO DUNIANI KWA KUPANDA MICHE 1000

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Taasisi za umma na binafsi waadhimisha siku ya mikoko duniani kwa kupanda miche takribani 1,000 ya miti ya  Mikoko eneo la Kilongawima lililopo pembezoni mwa fukwe ya 'Mbezi beach'  Halmashauri  ya Kinondoni Manispaa ya Jijini Dar es.

Akizungumza mara baada ya zoezi la upandaji wa miche hiyo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Saad Mtambule amewataka wananchi kulinda na kithamini mikoko kwani Inamanufaa mkubwa katika kulinda ikolojoa ya bahari na viumbe hai waishio majini. 

Meneja wa Tafiti za Mazingira (NEMC) Dkt. Rose Sallema akiwa ameshika mche wa Mkoko tayari kwa kuupanda katika zoezi la upandaji Mikoko eneo la Kilongawima

Naye Dkt.Rose Sallema, Meneja wa Tafiti za Mazingira (NEMC) alipozungumza alisema mikoko ni rasilimali ya bahari inayotakiwa kutunzwa kwani inafaida kiuchumi,kijamii na kimazingira.

Viongozi na wadau wa Mazingira wakitazama hati miliki ya TFS kuashiria ulinzi wa eneo la Kilongawima lililopandwa takribani miti ya Mikoko 1,000

Naye Mkurugenzi Msaidizi, Maendeleo ya Misitu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii ndugu. Seleboni Mushi alipozungumza aliitaka  jamii kuzingatia Uhifadhi wa misitu ya Mikoko kwani husaidia kuhifadhi fukwe na hewa ukaa hivyo kusaidia kuhimili mabadiliko ya tabianchi.

Afisa Mazingira Mkuu Bi. Ritha Said akipanda mche wa Mkoko wakati wa zoezi la upandaji Mikoko eneo la Kilongawima 

Ameongeza kuwa ni Hifadhi ya viumbe hai na husaidia jamii hasa za Pwani katika kujipatia kipato.

Taasisi zilizoshiriki Maadhimisho hayo ni pamoja na TFS, WWF, IUCN, Wetland, Mwambao International Wawakilishi kutoka maeneo ya Pwani ya Kibiti, Kilwa na Mafia.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ndugu. Saad Mtambule akizungumza na washiriki wote waliopanda miche ya Mikoko katika eneo la Kilongawimakatika kuadhimisha Siku ya Mikoko duniani


Zoezi la upandaji miti katika eneo la kilongawima likifanyika ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mikoko Duniani inayoadhimishwa tarehe 26 Julai kila mwaka ambapo kwa Tanzania imeadhimishwa tarehe 4 kwa kupanda Mikoko.

NEMC INAENDELEA KUTOA ELIMU KWA WANAFUNZI NA WANANCHI KATIKA MAONESHO YA NANENANE JIJI MBEYA

Elimu ya Utunzaji wa Mazingira ikiendelea kutolewa kwa wananchi na wanafunzi wa Sekondari ya Lyoto waliotembelea Banda la NEMC lililopo katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya.





MATUKIO KATIKA PICHA

Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Njombe Ndug. Christopher Aloyce Sanga  wakwanza kulia akipatiwa Elimu ya Utunzaji Mazingira baada ya kutembelea Banda la NEMC katika Maonesho ya Nanenane 2025 yanayofanyika Viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya. Karibu banda la NEMC upate elimu ya Mazingira kwa kilimo endelevu na rafiki kwa Mazingira.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Njombe Ndug. Christopher Aloyce Sanga alipotembelea banda la NEMC katika maonesho ya wakulima, nanenane 2025 jijini Mbeya 

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Songwe, Kidato cha Tano na cha Sita wametembelea Banda la NEMC katika maonesho ya Wakulima (Nanenane 2025) na kupatiwa elimu ya Utunzaji wa Mazingira ikiwa ni pamoja na elimu ya Utunzaji wa Mazingira inayoenda sambamba na Kilimo endelevu na rafiki kwa Mazingira, Kwa Jijini Mbeya maonesho ya Nanenane yanayofanyika Viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Songwe wakiwa katika banda la NEMC ambapo wamepatiwa elimu ya Utunzaji wa Mazingira katika maonesho ya nanenane 2025 jijini Mbeya 

NEMC IKO KAZINI- ELIMU YA MAZINGIRA YAENDELEA KUTOLEWA VIWANJA VYA NANENANE - DODOMA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizinw Mazingira (NEMC) limeendelea kuelimisha umma wa watanzania umuhimu wa kufanya kilimo, uvuvi na ufugaji salama unaozingatia misingi ya utunzaji Bora wa ardhi kwa maendeleo ya mazingira nchini.

Elimu hiyo inatolewa katika maonesho ya wakulima nanenane jijini Dodoma katika viwanja vya nzuguni yenye kaulimbiu isemayo " Chagua viongozi Bora kwa maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi"


Timu ya NEMC ikiendelea na utoaji wa elimu ya Mazingira katika maonesho ya Wakulima, nanenane 2025 katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma 

NEMC inaendelea kuwakaribisha wadau wote wa Mazingira katika Banda lao lililopo viwanja vya Nanenane, nzuguni Dodoma, kwenye hema la tatu la Taasisi za Serikali ili kupata elimu ya mazingira kwa maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi.



Wageni waliotembelea banda la NEMC katika maonesho nanenane 2025 wakisikiliza kwa makini elimu ya Mazingira inayotolewa na maafisa wa NEMC 


PROFESA MSOFE AZURU BANDA LA NEMC MAONESHO YA NANENANE- DODOMA

Naibu katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msofe ametembelea Banda la NEMC lililoko viwanja vya  Nanenane Nzuguni , Jijini Dodoma.

Akiwa bandani hapo, alifurahishwa na elimu ya Mazingira inayotolewa hususani ya namna bora ya kufanya kilimo, uvuvi na ufugaji unaozingatia utunzaji wa mazingira kwa mstakabali wa maendeleo endelevu nchini.

Amefurahishwa na huduma hiyo na kuitaka NEMC kuendeleza juhudi za utoaji elimu ya usimamizi na uhifadhi wa mazingira kwa mujibu wa Sheria

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, (Mazingira) Profesa Peter Msofe akizungumza na watumishi wa NEMC alipotembelea banda la NEMC leo 2 Agosti, 2025 katika maonesho ya wakulima (Nanenane 2025) yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma 

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Profesa Peter Msofe akisaini kitabu cha wageni  alipotembelea banda la NEMC katika maonesho ya wakulima (Nanenane 2025) yanayofanyika katika  Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma leo 2 Agosti, 2025



NEMC YASHIRIKI MKUTANO WA SABA WA UMOJA WA MATAIFA KUHUSU MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linashiriki Mkutano wa Saba (07) wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (07th Unit...