Nyumbani

NEMC YASHIRIKI UZINDUZI WA MFUMO WA KIDIGITALI WA KUFUTILIA UCHAFUZI WA MAZINGIRA ULIOFANYIKA MJINI ACCRA NCHINI GHANA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki uzinduzi wa mfumo wa kidigitali wa kufuatilia uchafuzi wa mazingira (Online Continuous Emissions Monitoring System) ambao umelenga kurahisisha upatikanaji wa taarifa za uchafuzi.

Uzinduzi huo uliofanyika tarehe 29 Julai 2025 mjini Accra nchini Ghana umehudhuriwa na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza Dkt. Immaculate Sware Semesi pamoja na Bi. Jackline Nyantori, Afisa Sheria Mkuu.

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi (katikati) akiwa na baadhi ya washiriki wa uzinduzi wa mfumo huo


Washiriki wa uzinduzi wa mfumo wa kidigitali wa kufuatilia uchafuzi wa Mazingira wakiwa katika Ukumbi ulipofanyika uzinduzi huo

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi (wa katikati) akiwa na baadhi ya washiriki wa uzinduzi wa Mfumo huo


Picha ya pamoja ya baadhi ya washiriki wa uzinduzi wa Mfumo huo 


NEMC YAPIGA MARUFUKU UCHIMBAJI WA MCHANGA MTO MPIJI KUEPUSHA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC leo 30 Julai, 2025 limepiga maarufu zoezi la Uchimbaji mchanga katika bonde la mto Mpigi unaotenganisha Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani ambalo limekuwa likiharibu Mazingira na kuhatarisha makazi ya watu wa eneo hilo kutokana na mmomonyoko wa udongo.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa mto huo, Meneja Uzingatiaji wa Sheria NEMC Bw. Hamadi Taimuru amesema ni marufuku wote wanaojihusisha na Uchimbaji wa mchanga katika mto huo kwa kigezo cha kusafisha mto. Amewataka kuacha mara moja uchimbaji na kuwataka wafike katika Ofisi za NEMC ili wapatiwe vibali vyenye vigezo vya kusafisha mto na si Uchimbaji wa mchanga kwa mustakabali wa utunzaji wa Mazingira.

Meneja Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bw. Hamadi Taimuru akitoa maelekezo ya marufuku ya uchimbaji mchanga katika mto mpiji wakati wa ziara ya ukaguzi wa mto huo

Amesema kwa mujibu wa Sheria, ni maarufu kuchimba mchanga mita sitini ndani mtoni kwani husababisha athari kubwa kwa Mazingira na hatari kwa makazi zikiwemo kuhama kwa mto, mmomonyoko wa udongo na kusababisha mafuriko ambayo ni hatari kwa makazi ya watu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Baraza la wazee Bw. Lazaro Silla amesema kwa niaba ya wakazi wa eneo hilo hawahitaji Uchimbaji wa mchanga katika eneo hilo kwani unasababisha uharibifu wa Mazingira na kuhatarisha usalama wa makazi yao hivyo ameiomba NEMC kudhibiti swala hilo ili lisiendelee kuleta madhara.

Timu ya NEMC ikiwa katika ziara ya ukaguzi wa mto Mpiji

Aidha, Bw. Taimuru ameongeza kuwa marufuku hii si tu kwa mto mpiji bali ni mito yote na maeneo yote nchini ambayo wanajihusisha na uchimbaji mchanga na kusababisha uharibifu wa Mazingira na kuhatarisha makazi ya watu.

Sambamba na hayo amesisitiza wote wanaojihusisha na Uchimbaji mchanga holela kote nchini kutii agizo hilo ili kuepusha uharibifu wa Mazingira na hatari ya kuharibika kwa makazi ili kujiepusha na adhabu kali inayoweza kutolewa.

Meneja Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bw. Hamadi Taimuru akitoa maelekezo ya marufuku kwa baadhi ya wachimbaji mchanga katika mto Mpiji 




NEMC NA ECCT WAHITIMISHA WANAFUNZI WA MRADI WA ECOWEAR

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC kwa kushirikiana na Taasisi ya ECCT (Environment Conservation Community of Tanzania) wamehitimisha takribani wanafunzi 22 wa Mradi wa '𝗘𝗰𝗼𝘄𝗲𝗮𝗿' waliokuwa wakipatiwa mafunzo yaliyobeba agenda ya mazingira kwenye ubunifu na Sanaa ya mitindo yenye lengo la kujenga ujasiliamali wa kijani, kupambana na taka ngumu za Sekta ya nguo na mitindo sambamba na matumizi endelevu ya rasilimali.

Mafunzo ya Mradi huo yalijikita kufundisha juu ya ubunifu wa bidhaa mbalimbali kupitia nguo zilizotumika na mabaki ya vitambaa ambapo ni  Utekelezaji wa dhana ya 𝗣𝘂𝗻𝗴𝘂𝘇𝗮, 𝗧𝘂𝗺𝗶𝗮 𝘁𝗲𝗻𝗮 𝗻𝗮 𝗥𝗲𝗷𝗲𝗹𝗲𝘇𝗮  kwa mustakabali wa utunzaji wa Mazingira na fursa za kiuchumi.

Akizungumza katika mahafali hiyo, mgeni rasmi, Meneja Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bi. Amina Kibola kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi ameipongeza Taasisi ya ECCT na wahitimu wote kwa kufanikisha mafunzo hayo na kuwataka kuyazingatia kwa manufaa ya kiuchumi na Mazingira.


Picha ya pamoja ya wahitimu, mgeni rasmi pamoja na viongozi wa Mradi huo mara baada ya kumalizika kwa hafla ya mahafali hayo

"Mmepata elimu, ujuzi, maarifa, mmeelewa changamoto za mazingira, sasa ni wakati wa kupeleka hayo yote kwa jamii zetu.Tuna matarajio makubwa kwenu kama mabalozi wa mitindo endelevu na watetezi wa mazingira. endeleeni kushirikiana, kushirikishana maarifa na kuamini kuwa sauti zenu na kazi zenu zinaweza kuleta mabadiliko." Alisisitiza Bi. Amina.

Bi. Amina pia ametumia fursa hii kutoa elimu kuhusu katazo la vifungashio vya plastiki kwa mujibu wa kanuni ya katazo hilo na kuwataka wahitimu wa Mradi huo kubuni na kutengeneza vifungashio vinavyoenda sambamba na mustakabali wa utunzaji wa Mazingira.

Mgeni rasmi, Meneja Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bi. Amina Kibola akizungumza katika mahafali hayo

Baadhi ya wahitimu wa Mradi wa ECOWEAR katika mahafali hayo

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa ECCT, Bi. Lucky Michael amelishukuru Baraza kwa mchango wake kufanikisha kuhitimisha wanafunzi hao huku akiainisha mafanikio ya Mradi huo ikiwa ni pamoja na kujengea uwezo wanafunzi hao ubunifu na mitindo,kukusanya takribani tani 2 za mabaki ya nguo na vitambaa kuzigeuza kuwa bidhaa zenye ubora pamoja na kuhamasisha jamii kupunguza taka na kutumia mitindo endelevu.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya ECCT Bi. Lucky Michael akizungumza katika mahafali hayo


Wahitimu wa Mradi wa ECOWEAR wakionesha baadhi ya kazi zao ambazo ni matokeo ya mafunzo ya Mradi 




NEMC YASHIRIKI MAFUNZO YA MBINU ZA KIJOGRAFIA KATIKA UCHAMBUZI WA TAARIFA ZA KIMAZINGIRA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki mafunzo ya muda mfupi yaliyolenga  kukuza uelewa kwa wataalamu katika umuhimu wa kutumia mbinu za Kijiografia (Geospatial Methods) kwenye uchambuzi wa taarifa za Kimazingira na Mabadiliko ya Tabia Nchi (Advanced GIS Training) yaliyoratibiwa na Shirika la Grumeti Fund Trust kupitia Programu ya Utafiti na Ubunifu kwa Mfumo Ikolojia wa Serengeti (Research and Innovation for the Serengeti Ecosystem-RISE).

Mafunzo haya yaliyoendeshwa kwa ushirikiano wa RISE, Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Chuo Kikuu cha Pennsylvania na Chuo Kikuu cha Montana yamefanyika ndani ya Hifadhi ya Grumeti, Magharibi mwa Serengeti kuanzia tarehe 14 hadi 20 Julai, 2025.






NEMC NA MAZINGIRA PLUS WAFANIKISHA PROGRAMU YA TAKA SIFURI KWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA YA DAR ES SALAAM

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) leo  25 Julai, 2025 kwa kushirikiana na Taasisi ya Mazingira Plus wamekabidhi Mradi wa Taka Sifuri kwa Shule ya Sekondari  maalumu ya wasichana ya Dar es Salaam ambapo takribani wanafunzi 200 wamehitimu na kukabidhiwa vyeti vya mafunzo ya Mradi huo.

Hafla hiyo ya kukabidhi Mradi huo iliambatana na maonesho mbalimbali ya matokeo ya mafunzo hayo ikiwa ni pamoja na bustani za kioganiki zilizotengenezwa na wanafunzi, utengenezaji wa mbolea kupitia mabaki ya chakula, mabanda ya kuhifadhi na kutenganisha taka pamoja na sanaa ya vinyago vilivyoonesha namna viumbe hai wanavyoathirika na uharibifu wa Mazingira.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi Mradi huo, Meneja Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bi. Amina Kibola amewapongeza wanafunzi hao kwa kuhitimu mafunzo hayo adhimu huku akiwasisitiza kuzingatia mafunzo hayo kwani yamebeba fursa za kiuchumi sambamba na Utunzaji wa Mazingira.

Meneja Uzingatiaji wa Sheria (NEMC) Bi. Amina Kibola akielezea dhana ya 'Punguza, Tumia tena na Rejeleza' katika hafla hiyo 

Aidha, Bi. Amina amewasisitiza kuzingatia dhana ya punguza, tumia tena na rejeleza ambayo ni msingi wa kudhibiti uchafuzi wa Mazingira na pia ni dhana ya kuibua fursa za kiuchumi kupitia urejelezaji wa taka na uchakataji wa taka kuwa malighafi kama vile mbolea.

Kwa upande wake Mratibu wa Programu ya Taka Sifuri mashuleni Bw. Suleman Mang'uro amewataka walimu wa Shule hiyo kusimamia na kuhakikisha Mradi huo unaendelea kwa manufaa ya kiuchumi na utunzaji wa Mazingira.


Afisa wa Taasisi ya Mazingira Plus akielezea maonesho ya sanaa za vinyago vinavyoonesha namna Uchafuzi wa Mazingira unavyoathiri viumbe hai

Picha ya pamoja baada ya hafla ya kukabidhi Mradi wa Taka Sifuri 



NEMC NA WIOMSA WAENDESHA WARSHA KUHUSU UMUHIMU WA VYAKULA VYA BULUU KATIKA LISHE NA USALAMA WA CHAKULA

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Taasisi ya WIOMSA (West Indian Ocean Marine Science Association) wameendesha Warsha kwa wadau wa Sekta mbalimbali za Serikali, binafsi na Sekta za kijamii kuhusu mchango wa vyakula vya baharini, mitoni na maziwa "Blue foods" katika lishe na usalama wa chakula.

Warsha hiyo ya Siku mbili imefanyika kuanzia tarehe 21 hadi 22 Julai, 2025 katika Ukumbi wa Hoteli ya Tanga Resort Mkoani Tanga.

Akizungumza katika ufunguzi wa Warsha hiyo Mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa buluu na Uvuvi Zanzibar Bw. Zahor Kassim Mohamed ameeleza kuwa vyakula vya buluu "Blue foods" ni muhimu sana katika lishe bora na usalama wa chakula.

"Vyakula vya buluu "Blue foods" kama vile samaki, dagaa, kaa, majongoo wa baharini, mwani na viumbe wengine vinamchango mkubwa katika lishe bora, usalama wa chakula, uchumi wa Kaya na ajira." Amesema Bw. Zahor Mohamed.

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akizungumza wakati wa Warsha  

Akiongea na Waandishi wa habari mara baada ya awamu ya kwanza ya Warsha hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi amesema lengo kuu la Warsha hii ni kuhamasisha juu ya umuhimu wa vyakula vya baharini,  katika mito na maziwa "Blue foods" katika lishe bora kwani vyakula hivyo vinamanufaa makubwa katika Afya ya mwanadamu na hivyo kujenga Taifa lenye watu wenye uelewa na kuweza kujitegemea.
Akiwasilisha mada Mkurugenzi wa Taasisi ya WIOMSA Dkt. Arthur Tude amesema  Taasisi hiyo imejikita katika tafiti za kuboresha lishe bora na kuelimisha jamii kuhusu vyakula vya baharini, hivyo imeamua kushirikiana na NEMC Pamoja na Taasisi nyinginezo kuhamasisha jamii juu ya uvunaji wa vyakula vya baharini vyenye lishe bora.


Aidha, Zahor alisisitiza kuwa ni muhimu Sekta zote binafsi na za Serikali, Taasisi na washirika wa maendeleo na jamii za uvuvi kuhakikisha kuwa "blue food" zinachangia kwa ufanisi kutokomeza njaa, kuongeza kipato na kulinda Mazingira ya bahari, mito na maziwa ambavyo ni rasilimali muhimu za kufuga vyakula buluu.

Ameongeza kuwa, licha ya changamoto zinazokabili ustawi wa vyakula vya buluu, Serikali imeweza kuimarisha Sekta hiyo ikiwa ni pamoja na kuwezesha ufugaji samaki katika mabwawa ya kisasa, kuwezesha vikundi vya Wanawake na vijana katika mnyororo wa thamani wa mazao ya maji, kushiriki katika juhudi za kimataifa za na kikanda kama vile Blue Economy na mabadiliko ya mifumo ya chakula duniani.


Washiriki wa Warsha wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya awamu ya kwanza ya warsha hiyo.

NEMC YATUNUKU TUZO KWA TANTRADE UTUNZAJI WA MAZINGIRA MSIMU WA SABASABA

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi akikabidhi tuzo hiyo, kwa Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE Bi.Latifa Khamis


Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetunuku tuzo ya heshima kwa Mamlaka ya maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuhusu utunzaji wa Mazingira, katika hafla ya kufunga maonesho ya biashara kimataifa  ya 49  iliyofanyika Jijini Dar es Salaam leo


Akikabidhi tuzo hiyo, kwa Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE Bi.Latifa Khamis,  Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi amesema NEMC imekabidhi tuzo hiyo kwa kutambua tano bora za utunzaji na usafi wa Mazingira uliosimamiwa nao katika kipindi chote cha Maonesho ya sabasaba 2025.



Dkt. Semesi amezianisha tano Bora hizo ambazo ni;

Ubunifu siku ya maalumu ya Mazingira ambayo iliadhimishwa tarehe 06.07.2025, mandhari ya maonesho kuwa safi na ya kupendeza kipindi chote cha Maonesho, kuhamasisha matumizi ya Nishati safi, kuhamasisha washiriki kutumia bidhaa ambazo ni rafiki kwa Mazingira na kufaulu kudhibiti taka licha ya idadi kubwa ya watu kutembelea maonesho hayo.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Saidi Jafo akizungumza

Hafla hiyo imehudhuriwa na Viongozi mbalimbali Wakuu wa Serikali akiwemo Waziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Kassim Majaliwa ambaye ndiye mgeni rasmi na aliyefunga maonesho ya sabasaba 2025, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Seleman Jafo pamoja na Viongozi wengine mbalimbali wa Serikali.


Maonesho ya biashara kimataifa kwa mwaka 2025 yamebeba Kaulimbiu mbiu isemayo "𝙈𝙖𝙤𝙣𝙚𝙨𝙝𝙤 𝙮𝙖 𝙗𝙞𝙖𝙨𝙝𝙖𝙧𝙖 𝙮𝙖 𝙆𝙞𝙢𝙖𝙩𝙖𝙞𝙛𝙖 𝙎𝙖𝙗𝙖𝙨𝙖𝙗𝙖, 𝙁𝙖𝙝𝙖𝙧𝙞 𝙮𝙖 𝙏𝙖𝙣𝙯𝙖𝙣𝙞𝙖".

Aidha, yamehudhuriwa na takribani nchi 22 na asilimia 70 ya wawekezaji wameweza kufikia malengo yao na kuongeza idadi ya wadau na masoko.


Baraza linaendelea kuhimiza wawekezaji na watanzania wote kwaujumla  kuendelea kuzingatia kanuni na miongozo ya utunzaji wa Mazingira kwa ajili ya Tanzania endelevu, safi na salama

PROFESA MSOFE AZURU BANDA LA NEMC MAONESHO YA NANENANE- DODOMA

Naibu katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Peter Msofe ametembelea Banda la NEMC lililoko viwanja vya  Nanenane Nzuguni ...